Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza:- Je, lini Serikali itatekeleza mradi wa maji wa Darakuta – Magugu - Mwada hadi Minjingu – Babati?

Supplementary Question 1

MHE. DANIEL B. SILLO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, pamoja na majibu ya Serikali napenda kujibu swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, yapita miaka miwili sasa toka Serikali ipeleke mabomba katika Miji Midogo ya Dareda na Galapo kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu ya maji chakavu.

Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya kukarabati miradi hii chakavu katika Miji hii ya Galapo na Dareda?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Daniel Sillo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, miundombinu chakavu katika maeneo aliyoyataja tayari Mamlaka ya BAWASA inashughulikia na imeomba fedha milioni 511 ya kufanya kazi hii ambayo imekatishwa watu wa Plasco lakini vilevile kuhakikisha maeneo chakavu yanafanyiwa kazi.

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza:- Je, lini Serikali itatekeleza mradi wa maji wa Darakuta – Magugu - Mwada hadi Minjingu – Babati?

Supplementary Question 2

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa kuwa Kiteto tumekosa vyanzo vya uhakika vya maji, ni lini Serikali itatuletea mradi wa Simanjiro ufike Kiteto?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge Olelekaita, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi wa Simanjiro kuelekea Jimboni kwake taratibu zinaendelea uhakikisha mara tukipata fedha tutaweka mkakati maalum kuhakikisha tunapeleka kule maji ya uhakika.