Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 2 Water and Irrigation Wizara ya Maji 26 2023-11-01

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza:-

Je, lini Serikali itatekeleza mradi wa maji wa Darakuta – Magugu - Mwada hadi Minjingu – Babati?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Daniel Baran Sillo, Mbunge wa Jimbo la Babati Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi wa maji Darakuta-Magugu ndiyo unaoendelezwa kwa awamu ya pili mpaka Minjingu ambapo utagharimu shilingi bilioni 5.672 na kazi zinazotarajiwa kufanyika ni pamoja na ulazaji wa bomba kuu umbali wa Kilometa 46, ujenzi wa tenki la lita 250,000 na ufungaji wa pampu za kusukuma maji. Utekelezaji wa mradi huu ulianza mwezi Juni, 2022 chini ya Mzabuni Plasco Limited na kazi hiyo ilitarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2023.

Mheshimiwa Naibu Spika, tarehe 3 Julai, 2023, Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Babati (BAWASA) ilivunja Mkataba na Plasco Limited baada ya kushindwa kukamilisha kazi kwa wakati. Kwa sasa, Serikali imeanza ununuzi wa mabomba kupita mfumo mpya wa Ununuzi wa NEST, na ifikapo mwezi Desemba 2023, Mzabuni wa mabomba atakuwa ameshapatikana.

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi huo utatekelezwa kwa muda wa miezi sita na unatarajiwa kukamilika tarehe 30 Juni, 2024 na utanufaisha wananchi zaidi ya 23,000 wa Kata za Mwada na Nkaiti.