Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Aloyce John Kamamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Chuo cha VETA Wilayani Kakonko?

Supplementary Question 1

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwanza naishukuru sana Serikali kwa majibu mazuri, niliomba kujengewa chuo na sasa ujenzi umeanza, naishukuru sana Serikali. Nina maswali mawili madogo ya nyongeza:

Mheshimiwa Naibu Spika, majengo ambayo yameanza kujengwa katika chuo kile ni majengo Tisa kati ya majengo mengi ambayo yatajengwa katika eneo hilo; Je, ni lini majengo hayo ambayo yapo katika mpango huo yataaanza kujengwa?

Swali la pili; ni lini ujenzi sasa utakamilika ili wananchi wa Wilaya ya Kakonko ambao wanasubiri chuo hiki kwa hamu sana utakamilika na mafunzo yaweze kuanza? Ahsante sana.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kamamba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli ujenzi wa vyuo hivi unagharimu zaidi ya shilingi bilioni tatu, kwa awamu ya kwanza tumetenga zaidi ya bilioni 1.5 kwa ajili ya majengo ya awamu ya kwanza ambayo ni majengo tisa na ujenzi huo umeanza mwezi wa Nane mwaka huu na ni ujenzi ambao tunatarajia utachukua kati ya miezi nane mpaka 12. Kwa hiyo, ni matarajio yetu ifikapo mwezi wa Sita au wa Saba mwakani majengo haya Tisa ya awamu ya kwanza yatakuwa yamekamilika na yatakapokamilika kwa sababu tumejenga kimkakati, tutahakikisha kwamba majengo haya yatakapokamilika chuo kiweze kuanza kutoa huduma hapohapo wakati tunaendelea na ujenzi wa awamu ya pili. kwa hiyo ujenzi wa awamu ya kwanza unatarajiwa kunako mwezi wa Sita, ama mwezi wa Saba mwakani utakuwa umekamilika then tutaanza ujenzi wa awamu ya pili kwa kadri ya upatikanaji wa fedha utakavyoruhusu. Nakushukuru