Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakuwa tayari kujenga Bwawa la Yongoma ambalo lilifanyiwa michoro ya awali mwaka 1984?

Supplementary Question 1

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nina swali la nyongeza; kwa kuwa Bwawa la Kalemawe lililopo Jimbo la Same Mashariki lililojengwa na wakoloni mwaka 1958/1959 limejaa tope sana na hili lilikuwa linasaidia sana wakulima wa kata ya Kalemawe, Kihurio na Bendera. Je, Serikali ina mpango gani kusaidia kutoa tope hilo ili ikusanye maji ya kuweza kusaidia kwenye kilimo cha umwagiliaji?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Naghenjwa Livingstone Kaboyoka, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaelekeza timu ya wataalam waende kuangalia eneo hilo ili wapate tathmini halisi na baadaye waweze kufanya utekelezaji katika eneo hilo.

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakuwa tayari kujenga Bwawa la Yongoma ambalo lilifanyiwa michoro ya awali mwaka 1984?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali la nyongeza.

Katika Jimbo la Manyoni Mashariki tuna Bwawa la Mbwasa ambalo tayari upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ulishafanyika. Je, nini kauli ya Serikali kuhusu lini itaanza ujenzi wa bwawa hilo? Ahsante sana.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Pius Chaya, Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Bwawa la Mbwasa liliwekwa katika mpango kupitia Benki ya BADEA na hivi sasa tunajiandaa kwa ajili ya ujenzi wa bwawa lenyewe, lakini vile vile na skimu za umwagiliaji katika bajeti ya fedha ya mwaka 2023/2024.

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakuwa tayari kujenga Bwawa la Yongoma ambalo lilifanyiwa michoro ya awali mwaka 1984?

Supplementary Question 3

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Pamoja na ahadi ya Mheshimiwa Waziri kutembelea Jimbo la Kalenga ambalo najua Waziri ataifanya, lakini napenda kujua ni lini sasa atatupa fedha za haraka angalau turekebishe Bwawa la Wellu katika Kata ya Ruanda ili lisaidie wananchi pale katika kilimo cha umwagiliaji?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kiswaga, Mbunge wa Kalenga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamuahidi tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaelekeza timu ya wataalam kufika katika eneo husika, mimi mwenyewe pia nitafika, ili tuone hali halisi na tuone namna ya kuweza kuwakwamua wananchi katika eneo hilo kwa sababu tumejipanga kuhakikisha kwamba sekta hii ya umwagiliaji inachukua hasa kipaumbele katika bajeti yetu inayokuja. Kwa hiyo, nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge, mimi mwenyewe nitafika na wataalam watafika kuoa namna ya kuweza kuwa-rescue wananchi katika eneo hilo.

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakuwa tayari kujenga Bwawa la Yongoma ambalo lilifanyiwa michoro ya awali mwaka 1984?

Supplementary Question 4

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Jimbo la Ndanda tuna skimu mbili za umwagiliaji ambazo ni Mkwera, Kata ya Nanganga pamoja na Skimu ya Ndanda, skimu hizi ziko kama zimekuwa abandoned, sasa nimuombe Mheshimiwa Waziri, kwa sababu ya uwekezaji mkubwa ambao ulifanyika pale, nini malengo ya Serikali na skimu hizi mbili ili ziweze kufanya kazi iliyokusudiwa vizuri?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cecil Mwambe, Mbunge wa Ndanda, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja kati ya kazi kubwa ambayo tumeipa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji ni kuhakikisha inapitia miradi yote ya umwagiliaji nchini Tanzania kwa maana ya kufahamu status zake, tujue ipi inafanya kazi, ipi imekwama na ipi inahitaji namna gani iweze kutoka hapo ilipo iendelee kufanya kazi. Kwa hiyo, nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba siyo dhamira yetu kuiacha na kui-abandon miradi hiyo mikubwa ya umwagiliaji, tutaifanyia kazi kuhakikisha kwamba inafanya kazi ili tutimize lengo la kuwa na eneo kubwa la umwagiliaji hapa nchini.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakuwa tayari kujenga Bwawa la Yongoma ambalo lilifanyiwa michoro ya awali mwaka 1984?

Supplementary Question 5

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Bwawa la Bolutu lililopo Kata ya Masama Magharibi lilifanyiwa tathmini na kugunduliwa lina maji mengi sana, lakini Bwawa la Kikafuchini kwa Tito na lenyewe lina maji ya kutosha.

Je, Serikali ni lini itajenga mabwawa haya ili yaweze kuwasaidia wananchi wa Jimbo la Hai?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Saashisha Mafuwe, Mbunge wa Hai, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumepokea rai ya Mheshimiwa Mbunge, tutajielekeza katika eneo hilo sisi na wataalam wetu kuona namna ambavyo tunaweza tukayafanya mabwawa hayo yatumike kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji na wananchi waweze kunufaika. Kwa hiyo, nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge, maelekezo yangu ni kwamba mtaalam wetu wa pale Mkoa wa Kilimanjaro atafika kwa ajili ya kuangalia na kufanya tathmini na baadae tufanye utekelezaji.