Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 49 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 438 2022-06-22

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itakuwa tayari kujenga Bwawa la Yongoma ambalo lilifanyiwa michoro ya awali mwaka 1984?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Naghenjwa Livingstone Kaboyoka, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli, usanifu na uandaaji wa michoro ya awali ya Bwawa la Yongoma ulifanyika mwaka 1984 na Serikali kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japani (JICA). Bwawa hili litakapokamilika litaweza kuhudumia wananchi katika Vijiji vya Misufini, Ndungu, Makokane na Mpirani. Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Same ipo katika hatua ya awali ya kufanya mapitio ya upembuzi yanikifu na usanifu wa Bwawa la Yongoma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kukamilika kwa mapitio hayo, ujenzi wa bwawa hili utawekwa katika mpango wa ujenzi kwa mwaka wa fedha 2023/2024. Aidha, Serikali inaendelea kuimarisha Skimu za Umwagiliaji za Same ambapo kwa sasa imepeleka mitambo katika Skimu ya Ndungu kwa ajili ya kufanya ukarabati wa dharura. (Makofi)