Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ramadhan Suleiman Ramadhan

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. RAMADHAN SULEIMAN RAMADHAN aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga Ghati la Kisasa la Abiria kwenye Bandari ya Dar es Salaam?

Supplementary Question 1

MHE. RAMADHAN SULEIMAN RAMADHAN: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri amekiri mwenyewe kwamba, upembuzi yakinifu utakamilika Desemba, je, ni lini ujenzi utaanza rasmi?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili; je, ujenzi huo utazingatia kwa kiasi gani kuweka vifaa vya kisasa ili abiria wasikaguliwe na mbwa kama inavyofanyika sasa?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. DAVID M. KIHENZILE): Mheshimiwa Naibu Spika, nipende kumhakikishia Mheshimiwa Ramadhan Suleiman Ramadhan kama nilivyosema hapo awali. Hatua ya kwanza ambayo Serikali inafanya ni kufanya uthamini au upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ambao utaweza kutusaidia kujua nini kinapaswa kufanyika. Pia, mara baada ya kukamilisha hatua hiyo, hatua itakayofuatia itakuwa ni kuanza kufikiria au kuanza mchakato kwa ajili ya ujenzi. Kwa sababu, Serikali imeendelea kufanya maboresho makubwa sana kwenye bandari zetu nchini ikiongozwa na Bandari yetu kubwa ya pale Dar es Salaam.

Mheshimiwa Naibu Spika, namba mbili; kama nilivyojibu swali la kwanza, katika usanifu huu unaoendelea kwa ajili ya ghati letu jipya la Dar es Salaam, utaambatana pamoja na ufungaji wa mashine ya ukaguzi wa kisasa ambao utatumia teknolojia ya kisasa ya ukaguzi kwa ajili ya abiria na mizigo.