Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 2 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 19 2023-11-01

Name

Ramadhan Suleiman Ramadhan

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. RAMADHAN SULEIMAN RAMADHAN aliuliza:-

Je, lini Serikali itajenga Ghati la Kisasa la Abiria kwenye Bandari ya Dar es Salaam?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. DAVID M. KIHENZILE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ramadhan Suleiman Ramadhan, Mbunge wa Chakechake, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ya Awamu ya Sita inaendelea kuimarisha huduma kwa wananchi wake katika maeneo mbalimbali ya nchi, likiwemo Jiji la Dar es Salaam. Ili kuendeleza juhudi hizo, Serikali kupitia TPA inakamilisha kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi wa gati la kisasa kwenye Bandari ya Dar es Salaam, ambao hadi sasa upo katika hatua za mwisho na unatarajia kukamilika mwezi Desemba, 2023.

Mheshimiwa Naibu Spika, niendelee kumshukuru sana Mheshimiwa Ramadhan Suleimani Ramadhan na Waheshimiwa Wabunge kwa ujumla kwa kuendelea kufuatilia kero za wananchi katika maeneo yao. Serikali itaendelea kuboresha huduma hizo ili kuwawezesha wananchi kufanya kazi zao bila kikwazo chochote.