Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza: - Je, lini Serikali italipa fidia kwa wananchi 438 Waliofanyiwa uthamini kupisha upanuzi wa Kiwanja cha ndege Kilwa – Masoko?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu ya Serikali na nina maswali mawili ya nyongeza. Mchakato wa uboreshaji na upanuzi wa Kiwanja cha Ndege Kilwa Masoko ni wa muda mrefu sasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza; nataka Mheshimiwa Naibu Waziri, awahakikishie Watanzania, Wanakilwa na Bunge hili, je, mpango wa Serikali wa uboreshaji na upanuzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kilwa Masoko bado uko pale pale?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; Mheshimiwa Naibu Waziri amefika Kilwa Masoko mara kadhaa. Alifika mwezi Juni akiwa Mwenyekiti wa Kamati na akafika mwezi Agosti akiwa Naibu Waziri katika Sekta hii ya Uchukuzi na alikuja mahususi kwa ajili ya masuala haya ya kiwanja cha ndege.

Mheshimiwa Naibu Spika, pale kuna changamoto kadhaa, kwa wananchi wangu hawa 438 mpaka sasa bado hawajalipwa fidia. Je, yuko tayari sasa baada ya Bunge hili kwenda Kilwa Masoko akiambatana nami ili kwenda kusikiliza kero za hawa wananchi wangu 438?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. DAVID M. KIHENZILE): Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimpe uhakika Mheshimiwa Mbunge wa Kilwa Kusini kwamba, Serikali ya Awamu ya Sita inayo dhamira ya dhati ya kuboresha Uwanja wa Ndege wa Kilwa Masoko. Pia, hiyo inakwenda sambamba na uwekezaji mkubwa unaofanyika pale wa kujenga bandari kubwa kwa ajili ya uvuvi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, namhakikishia kwamba mpango wa Serikali uko pale pale, mara baada ya wenzetu wa Wizara ya Fedha kukamilisha taratibu za ndani, fidia hiyo kwa wananchi hao itaanza kulipwa. Hilo moja.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili anauliza je, niko tayari kuambatana naye baada ya kumaliza Bunge hili. Amekiri mwenyewe nilikwenda pale pamoja na wenzangu nikiwa Mwenyekiti wa Kamati Kilimo na Mifugo. Vile vile, nimekwenda hapo juzi kukagua bandari hiyo na uwanja huo. Niko tayari kwenda pamoja naye ili tukawape uhakika wananchi hao ambao wanamwamini Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ili waendelee kujenga imani naye.