Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 2 Works, Transport and Communication Wizara ya Uchukuzi 18 2023-11-01

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza: -

Je, lini Serikali italipa fidia kwa wananchi 438 Waliofanyiwa uthamini kupisha upanuzi wa Kiwanja cha ndege Kilwa – Masoko?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ally Mohamed Kassinge, Mbunge wa Kilwa Kusini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi cha robo ya mwisho wa mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali ilikamilisha zoezi la Uwekaji Wazi Daftari la Fidia (valuation report disclosure) kwa wananchi 438 waliofanyiwa uthamini ili kupisha upanuzi wa Kiwanja cha Ndege Kilwa Masoko.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na hatua hiyo, mnamo mwezi Agosti, 2023 Wizara ya Fedha ikishirikiana na Wizara ya Uchukuzi, Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) na Ofisi ya Ardhi Mkoa wa Lindi, walifanya na kukamilisha zoezi la uhakiki wa daftari la fidia.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya hatua hizi, zoezi la ulipaji wa fidia litaanza mara baada ya Wizara ya Fedha kukamilisha taratibu zote za kifedha.