Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itathibitisha Mkataba Na. 189 wa Wafanyakazi wa Majumbani?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Waziri kwa ushirikiano katika eneo hilo nimekuwa nikisaidia sana. Lakini swali langu la kwanza swala la wadau kutoa maoni pamoja na elimu limefanyika kwa muda mrefu sana.

Je, Serikali kupitia comissionar wa kazi haioni iko haja sasa ya kuharakisha kuridhia mkataba huo angalau wawe parcial ili wafanyakazi hao wawe rasmi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, baada ya Serikali kupitia VETA na CVM kuzindua mitaala ya wafanyakazi wa majumbani, je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza udahili wa wanafunzi hao kwa sababu sasa hivi hata wanafunzi kutoka Vyuo Vikuu na Vyuo vingine wanaajiriwa kufanya kazi majumbani. Ni mpango gani sasa Serikali inafanya ili wanafunzi wawe wengi katika hivyo Vyuo vya VETA? Ahsante. (Makofi)

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI) Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Thea Medard Ntara kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli mkataba huu wa kimataifa tayari Serikali ilikwisha kuanza kuchukua hatua toka mwaka 2021 lakini kwa sehemu kubwa kama Mheshimiwa Mbunge anavyoelewa na nampongeza sana amekuwa akipambana sana amekuwa akipambana sana kuhusiana na swala hili. Katika mikataba ya kimataifa ina hatua za msingi tatu, hatua ya kwanza ni ya ku-sign pale ambapo wanachama wa umoja huo wanapokutana.

Mheshimiwa Naibu Spika, hatua ya pili ni reservation na ya tatu ni lactification. Kwenye reservation ni pale ambapo nchi inaruhusiwa kutokukubaliana na baadhi ya matakwa ambayo yameelezwa lakini, katika ratification ni pale ambapo tayari mme-sign na badae mnaingia kwenye ratification kwamba mnaamua kuzi-domesticate hizo sheria ziweze kufanya kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kufanya hivyo pamoja na uchambuzi ambao umeeleza na wadau ambapo tuliwashirikisha tulibaini kwamba sisi tulikuwa mbele kidogo ya mkataba huu wa kimataifa wa mwaka 2011 kwenye masuala ya kazi, Sheria tayari sisi tunazo nchini ambazo zinaeleza utaratibu wa kazi lakini pia masuala ya mkataba na hatua nyingine maswala ya mishahara lakini pia masuala ya afya na usalama mahali pa kazi na masuala ya ifadhi ya jamii. Haya yote yapo yameelezwa kwenye mkataba lakini sisi tulikuwa tumekisha kuyafanyia kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaenda kuangalia sasa yale ambayo yatakuwa yanautofauti na ambayo yatakuwa na tija kwa upande wetu. Kwa kweli kundi hili ni muhumu na tunaendelea kulihudumia.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili la kuhusu mtaala wa wafanyakazi. Ni kweli Serikali ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan iliona umuhimu wa wafanyakazi wa ndani kuwa wananyanyasika sana na kwa Sheria tuliyonayo katika Kifungu cha tano cha Sheria ya Ajira na mahusuano kazini, Kifungu cha sita, cha saba lakini pia kifungu cha 11, vyote hivi vinaeleza kuhusu haki na wajibu wa wafanyakazi hawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia kwa sababu tumeanzisha hiyo program kwenye Vyuo vya VETA wewe mwenyewe utakuwa shahidi na Waheshimiwa Wabunge kwamba wafanyakazi wa ndani wananyanyasika sana kwenye maeneo mengi. Sasa tumeona kuanzisha utaratibu huo wa taaluma na kutangaza zaidi ili udahili uongezeke lakini pia kuhakikisha wanafanya kazi kimikataba na watambue na hata sisi kama wawakilishi…