Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 2 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu 8 2023-11-01

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itathibitisha Mkataba Na. 189 wa Wafanyakazi wa Majumbani?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Thea Medard Ntara, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, hatua ya kuridhia Mkataba Na. 189 ulianza mwaka 2011 hadi 2016 ambapo ulifika hatua ya kuridhiwa kwa kuwasilishwa Bungeni. Hata hivyo, kwa kuzingatia maslahi mapana ya nchi na utekelezaji wa Mkataba tajwa, iliamuliwa kuwa wadau waendelee kupewa elimu kuhusu Mkataba huo kabla ya hatua za uridhiaji kuendelea. Hivyo, Serikali kwa kushirikiana na Chama cha Wafanyakazi wa Majumbani CHODAWU imetoa elimu kuhusu Mkataba husika kupitia Makongamano na vikao 90 ambao ni wafanyakazi wa majumbani, Viongozi wa vyama vya wafanyakazi na waajiri.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka 2023/2024, Serikali imeanza hatua ya uchambuzi wa Mkataba Na. 189 kwa kupitia Sheria na Kanuni zinazosimamia wafanyakazi wa majumbani. Baada ya hatua hizo na mapitio kukamilika, hatua inayofuata ni ya kushirikisha wadau kwa lengo la kupokea maoni yao kuhusu maeneo ambayo Serikali inapendekeza kuridhia katika mkataba husika. Aidha, Serikali itazingatia umuhimu wa vipengele vya mkataba ambavyo vitazingatia mila, desturi na uwezo wa nchi katika kutekeleza Mkataba husika, ahsante. (Makofi)