Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga minara ya simu katika Makao Makuu ya Halmashauri ya Msalala?

Supplementary Question 1

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Spika, ahsante, ni lini sasa mtaanza ujenzi wa minara hii kwenye maeneo ambayo umeyataja?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; kwenye maeneo ambayo huduma ya 5G, naomba nirudie.

Mheshimiwa Spika, kwenye maeneo ambayo huduma ya 5G inapatikana kumekuwa na malalamiko mengi ya juu ya uwekaji wa bundle kwisha haraka. Sasa nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba wanatatua tatizo hili la kwisha bundle mapema? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Iddi Kassim Iddi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kipengele cha kwanza, kama ambavyo nimejibu katika jibu langu la msingi kwamba tayari Vodacom wako katika hatua mbalimbali za utekelezaji wa ujenzi wa mnara huo.

Mheshimiwa Spika, kwa kipengele cha pili, naomba nielezee kidogo; ni kweli kabisa, kwanza niseme jambo moja, Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na Serikali yake inawapenda sana Watanzania, na kupitia Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambayo ndio mlezi wa sekta ya mawasiliano nchini, kazi yetu ni kuhakikisha kwamba tunalinda na kutetea maslahi ya watoa huduma na watumiaji wa huduma. Hivyo, hatutapuuzia wala Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan haijawahi kupuuzia malalamiko ya wananchi.

Mheshimiwa Spika, hivyo basi, nitumie Bunge lako Tukufu kuwaagiza taasisi zetu mbili, taasisi ya kwanza ambayo ni Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) iliyoanzishwa kwa Sheria Namba 12 ya mwaka 2003 kwa kutumia kifungu cha 40 wakashughulikie malalamiko haya ya wananchi kuhusu changamoto za kuongezeka kwa malalmiko ya uongezaji wa bundle, lakini linaisha bila kuwa na taarifa rasmi.

Mheshimiwa Spika, lakini jambo lingine, tuna TCRA CCC; hii ilianzishwa pia kwa Sheria Namba 12 ya mwaka 2003 ambapo kupitia kifungu cha 37 inampa mamlaka ya kuhakikisha kwamba inalinda haki na maslahi ya watumiaji kwa huduma ya mawasiliano. Hivyo, wakalifanyie kazi hili na watoe ripoti Wizarani, ili sasa kama kutagundulika kwamba kuna changamoto za kiufundi, basi TCRA wakafanye kazi kwa mujibu wa sheria.

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga minara ya simu katika Makao Makuu ya Halmashauri ya Msalala?

Supplementary Question 2

MHE. FRANCIS I. MTINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante, Kata ya Kikonda, Kinampundu na maeneo ya Kata ya Ilunda yana shida sana ya mtandao. Ni lini Serikali inaenda kujenga mnara katika maeneo hayo?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, changamoto katika jimbo lake ilikuwa kubwa sana, lakini kuna baadhi ya maeneo ambayo tunayaingiza kwenye utekelezaji wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali, lakini katika kata hiyo ambayo Mheshimiwa Mbunge ameitaja, naomba niipokee ili tukaiingize katika utaratibu wa hatua zinazofuata kulingana na upatikanaji wa fedha, ahsante.