Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza:- Je, kuna mpango gani wa kutumia eneo la uwekezaji la Kisasiga – Bukene kutengeneza miundombinu ya Block Farms kwa kilimo cha alizeti?

Supplementary Question 1

MHE. SELEMANI J. ZEDI: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina swali la nyongeza. Shamba hili la Kisasiga lenye ukubwa wa ekari 48,000 zoezi la kupima udongo lilishafanyika na lilifanywa na watalamu wa Taasisi ya Kilimo ya TARI Mlingano tangu mwezi Agosti, 2021 na majibu yakaja kwamba shamba lile linafaa kwa Kilimo cha Alizeti. Kwa hiyo upimaji umeishafanyika, majibu yameishakuja.

Mheshimiwa Spika, sasa swali langu ni Serikali haioni kwamba sasa hivi kinachotakiwa ni kupeleka Watalam wa Miundombinu ya Ujenzi wa Block Farm ili washirikiane na Watalam wa Halmashauri ya Wilaya ya Nzega kufanya tathimini ya Ujenzi wa Miundombinu ya Block Farm ili mwaka huu wa fedha unaokuja ibaki tu kutafuta fedha ili kazi ya ujenzi wa block farm ianze kwa sababu ekari 48,000 zimekaa idle na majibu tangu mwaka 2021 yameishapatika. (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kama ambavyo tumejibu katika jibu la msingi kwamba kuna Timu ya Watalam wa Wizara na yenyewe imefika katika eneo la Nzega na baada ya hiyo taarifa hatua zote ambazo Mheshimiwa Mbunge amezisema Wizara itazifanyia kazi. Bahati nzuri sana katika kipindi ambacho Serikali ya Awamu ya Sita imewekeza msukumo mkubwa katika kilimo ni kipindi cha Dkt. Samia Suluhu Hassan. Nimthibitishie tu kwamba shamba hilo litajengwa na Watalam watapelekwa kwa ajili ya kufanya hiyo tathimini ya miundombinu na katika mwaka wa fedha tutaliweka katika bajeti, ahsante sana. (Makofi)