Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Anania Tadayo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Primary Question

MHE. JOSEPH A. TADAYO aliuliza:- Je, lini Serikali itatekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa Stendi ya kisasa katika Mji wa Mwanga?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH A. TADAYO: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, nina swali moja tu la nyongeza. Andiko la mradi liliwasilishwa tarehe 28 Desemba, 2021. Mwaka 2022 nilikumbushia kwa njia ya swali la nyongeza, nikapewa majibu kwamba mchakato unaendelea.

Mheshimiwa Spika, mwezi Julai, mwaka huu 2023 Mheshimiwa Deogratius Ndejembi, Naibu Waziri, TAMISEMI, alitembelea Jimboni kwangu, tulipomkumbushia hilo ndiyo akashauri kwamba tufanye wasilisho la kukumbusha. Kwa hiyo, wasilisho analoli-refer Mheshimiwa Waziri hapa ni la kukumbusha ambalo limewasilishwa mwezi Agosti mwaka huu 2023 na ninalo hapa, limefanya reference kwa andiko la msingi ambalo ni la mwaka 2021.

Mheshimiwa Spika, swali langu: Kwa kuwa hii ni ahadi ya Mheshimiwa Rais na ni ya muda mrefu: Je, Mheshimiwa Waziri sasa yuko tayari kutuambia ni lini kazi hii itaanza ili wananchi wa Mwanga waanze sasa na wao ku-¬play their party kwa kuanza kukusanya material site kama sehemu ya mchango wao?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Ni kweli kwamba Halmashauri ya Mwanga iliwasilisha andiko awali mwaka 2021, Ofisi ya Rais, TAMISEMI ilipitia na kuwarejeshea kwa ajili ya kuboresha maeneo ambayo yalihitaji maboresho zaidi. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, ahadi za viongozi wetu wa Kitaifa, ahadi za Mheshimiwa Rais ni kipaumbele chetu na ndiyo maana tayari tumeingiza kwenye mpango, tunafanya tathmini ya mwisho wa vigezo na wakati huo huo tunatafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi katika Halmashauri hiyo ya Mwanga.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, namwomba Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Mwanga wawe na imani kwamba Serikali kuna hatua za mwisho za tathmini na mara fedha zikipatikana tutakwenda kuanza ujenzi wa stendi hiyo, ahsante.

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. JOSEPH A. TADAYO aliuliza:- Je, lini Serikali itatekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa Stendi ya kisasa katika Mji wa Mwanga?

Supplementary Question 2

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Mwaka 2022 niliuliza swali hapa ndani ya Bunge nikajulishwa kwamba nilete andiko kwa ajili ya ujenzi wa Stendi ya Wilaya ya Biharamulo. Pia kwenye miradi ya kimkakati wa Mkoa wa Kagera kwenye bajeti ya mwaka huu 2023 tuliwasilisha pia. Sasa, naomba kujua ni lini ujenzi wa Stendi ya Wilaya ya Biharamulo utaanza ili wananchi wa Biharamulo waweze kupata huduma hiyo? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, nimpongeze Mheshimiwa Mbunge na Halmashauri ya Biharamulo kwa kuwasilisha andiko la maombi ya Mradi wa Ujenzi wa Stendi ya Halmashauri na nimwambie tu kwamba baada ya mawasilisho hayo Serikali inaendelea kupitia maandiko yale kufanya tathmini ya vigezo. Pia sambamba na hilo, kutafuta fedha kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimhakikishie tu kwamba, mara fedha zikishapatikana na baada ya kupitia andiko hilo na kujiridhisha na vigezo, fedha itatafutwa kwa ajili ya kujenga stendi hiyo ya Biharamulo, ahsante.

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. JOSEPH A. TADAYO aliuliza:- Je, lini Serikali itatekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa Stendi ya kisasa katika Mji wa Mwanga?

Supplementary Question 3

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi kuuliza swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, mwaka jana 2022 niliuliza swali na Mheshimiwa Naibu Waziri alinijibu kwa kutushauri kwamba tuandike andiko na tuwasilishe katika TAMISEMI kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Mabasi Wilaya ya Namtumbo: Je, Serikali nayo iko tayari au inaweza kutueleza ni lini nasi tutapata fedha kwa ajili ya kujenga stendi hiyo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Nimhakikishie Mheshimiwa Vita Kawawa kwamba Serikali inaendelea kutafuta fedha. Nafahamu Jimbo la Namtumbo na majimbo mengine yote kwa Waheshimiwa Wabunge, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa awamu, pia kupitia maandiko hayo ili baada ya hapo tuanze ujenzi wa vituo vya mabasi kwa awamu.

Mheshimiwa Spika, nitumie fursa hii kuwakumbusha Wakurugenzi wa Halmashauri kwamba pamoja na Serikali Kuu kutafuta fedha, lakini fedha za Serikali ni pamoja na fedha za mapato ya ndani. Kwa hiyo, ni wajibu wao kuanza kutenga fedha angalau kwa awamu, kujenga kila mwaka wa fedha wakati Serikali Kuu inatafuta fedha kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa stendi hizo, ahsante.