Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE K.n.y. MHE. MARTHA N. GWAU aliuliza: - Je, Serikali haioni kuna haja ya watoto wachanga kutumia Bima za Afya za Mama zao?

Supplementary Question 1

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, nina maswali madogo mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni juzi tu tumepitia Sheria ya Bima ya Afya, je, katika sheria hii, ita-consider mtoto ambaye anazaliwa kwa kadi ya mama yake kutumia angalau kwa miezi mitatu wakati wazazi wanajipanga kumtengenezea bima huyu mtoto aliyezaliwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili; Serikali ilishawahi kutoa tamko kama hili kwamba imeelekeza hospitali, wazazi wanapojifungua watumie bima za mama zao lakini hili halifanyiki. Nini kauli nyingine ya Serikali kwa sababu jambo hili linajirudia, Serikali inasemaje katika hili?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba kujibu maswali mawili mazuri ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Moja; anasema je, sheria iliyopo sasa ambayo tulipitisha juzi kwamba inaenda ku-accommodate, labda nisisitize tu, kwamba siyo tu sheria tuliyoipitisha juzi kuanzia sasa ni kwamba, watoto wanaozaliwa hospitali ambao wazazi wao wana kadi zao za bima, watibiwe na wapate huduma kwa sababu ambazo nimezielezea hapa inawezekana ku-track vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, akaseme je, tunafanya nini kuhusu ambao sasa wanakwenda kwenye vituo vyetu na tayari tulitoa tamko lakini bado hayo matatizo yanaendelea. Waheshimiwa Wabunge wenzangu ninawaomba pia nawaasa Watanzania wenzangu na ninawaasa Watumishi wa Mfuko wa Bima ya Afya na hospitali zote Tanzania kwamba sasa hivi tukisikia hilo na likitokea na Mheshimiwa Mbunge ukikutana na kitu kama hicho naomba utuletee na mtu huyo ambae amesababisha hayo atachukuliwa hatua mara moja palepale. (Makofi)