Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 4 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 61 2023-11-03

Name

Martha Nehemia Gwau

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE K.n.y. MHE. MARTHA N. GWAU aliuliza: -

Je, Serikali haioni kuna haja ya watoto wachanga kutumia Bima za Afya za Mama zao?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Afya, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Martha Nehemia Gwau, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kumekuwa kukitokea changamoto kwa wazazi wenye bima wanaojifungua watoto wao kushindwa kupata huduma hasa kwenye vituo vya huduma za afya vya sekta binafsi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri wa Afya alishatoa maelekezo kwa Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya kuhakikisha watoto wachanga wenye uhitaji wa huduma wanapata huduma za afya bila kikwazo chochote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kutumia fursa hii kuelekeza Watendaji wa Mfuko wa Bima ya Afya na vituo vyote vya huduma za afya nchini kuhakikisha watoto wanapata huduma kwani Mama yupo na kadi yake inayoonesha ushahidi wote kuhusu mtoto husika na ni mtoto wa ngapi kwenye familia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawaasa wazazi na viongozi wa hospitali husika kukomesha kabisa matukio ya kughushi nyaraka ambayo pia ndiyo yanapelekea kuwepo na usumbufu wakati mwingine. Naomba kuwasilisha.