Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY K.n.y MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga barabara ya lami kutoka Kawajense – Ugalla hadi Kahama?

Supplementary Question 1

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina maswali mawili. Swali la kwanza; je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kuweka fedha kwenye bajeti ijayo ili Barabara hii ya Ugalla - Kahama ikawa kwenye bajeti kwa uhakika?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; Barabara ya Dareda - Dongobesh aliiweka kwenye mpango wa kujengwa kwa kilomita tisa na mpaka leo haijaanza kujengwa. Je, ni lini ujenzi wa barabara hiyo utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara niliyoitaja kuna baadhi ya maeneo ambayo yalikuwa hayajafunguliwa, kwa hiyo kitu cha kwanza ni kuifungua yote na kuikamilisha. Pia tuliona kwanza tufanye usanifu uliokamilika kwenye Daraja kubwa la Mto Ugalla, lakini kabla ya kufika kwenye Daraja la Mto Ugalla kuna madaraja madogo sita ambayo tumeanza kuyajenga ili kulifikia hilo daraja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tutakapokamilisha ujenzi wa hayo ma-culvert, hatua ya pili itakuwa ni kujenga hilo daraja ili kuifungua barabara yote ambayo inaunganisha Mkoa wa Katavi – Tabora na Mkoa wa Shinyanga kwa upande wa Kahama. Kwa hiyo, tutakapokuwa tumekamilisha hii kazi sasa Serikali itaweka kwenye bajeti kuijenga barabara yote, lakini cha muhimu kwanza ni kukamilisha hayo madaraja ili kwanza tuifungue hiyo barabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye swali lake la pili la Barabara ya Dareda – Dongobesh, ni kweli tulikuwa tumepata mkandarasi, lakini ikatokea tatizo la kimkataba ambalo sasa limeshatatuliwa na tunategemea kukamilisha manunuzi ya hiyo barabara. Baada ya hapo naamini barabara hiyo inaenda kujengwa kwa kiwango cha lami, ahsante.