Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 4 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 55 2023-11-03

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY K.n.y MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza:-

Je, lini Serikali itajenga barabara ya lami kutoka Kawajense – Ugalla hadi Kahama?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Anna Richard Lupembe, Mbunge wa Nsimbo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeanza maandalizi kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa Barabara ya Kawajense ambapo ni Mpanda – Ugalla – Kaliua – Ulyankulu – Kahama yenye urefu wa kilomita 456 ambapo kazi ya upembuzi yakinifu imekamilika na kazi itakayofuata ni kufanya usanifu wa kina. Aidha, usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi wa Daraja la Ugalla pamoja na madaraja saidizi sita yaani relief culverts umekamilika na kazi ya ujenzi wa madaraja hayo imeanza na inatarajia kukamilika mwaka 2024. Kwa sasa Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara hiyo, ahsante.