Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Vincent Paul Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. VINCENT P. MBOGO aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Masoko ya Kuuzia Samaki katika Kata za Ninde, Wampembe na Kala Wilayani Nkasi?

Supplementary Question 1

MHE. VINCENT P. MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Nina maswali mawili ya nyongeza. Ziwa Tanganyika, Wilaya Nkasi hakuna vizimba hata kimoja . Ni lini Serikali mtapeleka vizimba Wilaya ya Nkasi hasa Jimbo la Nkasi Kusini? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la namba mbili, lini Serikali itamalizia ujenzi wa Bwawa la Kacheche la kunyweshea mifugo pamoja na ujenzi wa majosho mawili Chala B, Kata ya Chala pamoja na Kijiji cha Kitosi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaanza na hili la vizimba, tumeshatoa maelekeza kwamba mvuvi yeyote ama mwananchi yeyote ambaye ana shida na vizimba ama boti au nyenzo zozote zinazohusiana na uvuvi, aombe haraka iwezekanavyo milango ipo wazi kwa Watanzania wote. Kwa kweli Mheshimiwa Rais, ametufungulia njia kama mnavyokumbuka Tarehe 30, aligawa kule Mwanza vizimba na boti za kutosha na Wizara ipo katika mchakato wakutafuta vizimba vingine ili kuwagawia wananchi watakaohitaji kwa awamu ya pili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimuombe Mheshimiwa Mbunge aendelee kuhamasisha Wananchi wake wenye uhitaji. Tupo tayari kupeleka Ziwa Tanganyika na tayari tumeshaanza Ziwa Victoria na kwa kweli vijana wote na wavuvi wote wenye shida na wenye uhitaji wa nyenzo za uvuvi Serikali ipo tayari kuwagawia. Ahsante. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili la pili, kuhusiana na lini bwawa litakamilika na majosho. Hapa katikati tulisimama kidogo kwa sababu ya upatikanaji wa fedha. Mara tu Serikali itakapopata fedha tutakwenda kukamilisha ujenzi wa majosho hayo. Mheshimiwa Mbunge atakumbuka katika Wilaya yake tumemtengea jumla ya shilingi bilioni 1.6 kwa ajili ya ujenzi wa soko la samaki katika eneo hilo. Tukapopata fedha nyingine tutakwenda kukamilisha ujenzi wa majosho hayo na mabwawa ambayo yapo katika Wilaya yake, ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Primary Question

MHE. VINCENT P. MBOGO aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Masoko ya Kuuzia Samaki katika Kata za Ninde, Wampembe na Kala Wilayani Nkasi?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. ANGELINE S. L. MABULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Ninashukuru kwa kunipa fursa na mimi niulize swali la nyongeza. Kwanza, ninashukuru kwa huduma tuliyoipata miundombinu katika Ziwa Victoria. Wilaya ya Ilemela asilimia 87 ni eneo la maji, na wanawake na vijana wengi wanashughulika na mazao ya samaki hususani dagaa lakini miundombinu yao ya kukausha samaki si mizuri hasa kwa afya ya binadamu. Ni lini Wizara itasaidia kuweka miundombinu kwa ajili ya kukausha samaki kwa wafanyabiashara hao? (Makofi)

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo nimesema kwamba Serikali imeshaanza na katika Ziwa Victoria tumeshaanza kuwasaidia Wavuvi namna ya kuvua zile samaki lakini pia kuhifadhi samaki. Hili wazo la Mheshimiwa Mbunge tumelichukua tutakwenda kulifanyia kazi kuwasidia Wavuvi wakanda ya ziwa. (Makofi)

Name

Simon Songe Lusengekile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. VINCENT P. MBOGO aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Masoko ya Kuuzia Samaki katika Kata za Ninde, Wampembe na Kala Wilayani Nkasi?

Supplementary Question 3

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwenye orodha ya masoko ya Samaki yatakayojengwa katika mpango ambao ameusema Mheshimiwa Naibu Waziri kwa mwaka wa fedha 2023/2024 ni pamoja na Nyamikoma, Jimbo la Busega. Mpaka sasa soko hili halijaanza kujengwa na imebaki miezi minne kukamilika kwa mwaka wa fedha. Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa soko hili la Nyamikoma? (Makofi)

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaanza ujenzi wa Soko Nyamikoma mara tu fedha zitakapokuwa zimepatikana. Tayari Serikali imeshaanza ujenzi wa masoko katika maeneo mbalimbali ikiwa ni pamoja na Tunduma, Muleba, Momba, Ludewa, Busega, Nkinga na Kalambo. Kwa hiyo, mara tu tutakapopata fedha Serikali itaanza ujenzi haraka sana iwezekenavyo katika Kijiji cha Nyamikoma. (Makofi)