Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 11 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 181 2024-02-13

Name

Vincent Paul Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. VINCENT P. MBOGO aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga Masoko ya Kuuzia Samaki katika Kata za Ninde, Wampembe na Kala Wilayani Nkasi?

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Vincent Paul Mbogo, Mbunge wa Nkasi Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kuboresha na kujenga miundombinu ya uvuvi katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo katika mwambao wa Ziwa Tanganyika. Katika mwaka 2023/2024, Serikali inajenga masoko ya samaki saba na mialo mitatu ambapo Wilaya ya Nkasi imepangiwa kujengewa mwalo wa Karungu. Aidha, Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeingia Mkataba na Mkarandarasi Nice Construction and General Supplies Ltd. wenye thamani ya shilingi bilioni 1.6 kwa ajili ya kujenga mwalo wa Karungu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwalo huo wa Karungu utakaojengwa utakuwa na miundombinu ya soko ikiwemo chumba cha ubaridi, mtambo wa kuzalisha barafu na sehemu ya kuuzia samaki. Aidha, nimuombe Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Nkasi kutumia miundombinu hiyo kwa pindi itakapokamilika wakati Serikali inatafuta fedha za kujenga masoko ya samaki katika kata zingine zilizosalia. Vilevile, Serikali itaendelea kujenga miundombinu ya uvuvi katika maeneo mbalimbali nchini kuendana na upatikanaji wa fedha na mahitaji ya maeneo husika.