Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, lini Kata za Tchenzema, Lingali, Kikeo na Lwale katika Tarafa ya Mgeta - Morogoro zitapatiwa umeme?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, licha ya kupeleka umeme katika Kata za Chenzema, Langala na hizo nyingine zote, naishukuru Serikali kwa sababu inachukua huduma sana kwenye umeme: Je, ni lini vijiji vya Kidunda pamoja na Ngolehanga vitaweza kupatiwa umeme? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ni lini vijiji na vitongoji vya Morogoro vijijini vitaweza kupata umeme? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII K.n.y. WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, naomba kujibu maswali ya Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Morogoro kwa ujumla wake una vijiji vilivyohitaji kupatiwa umeme takribani 668. Vijiji ambavyo vilikuwa vipo katika mpango wa kupelekewa umeme ni vijiji 239. Mpaka sasa tumeshapeleka umeme kwenye vijiji takribani asilimia 90. Makusudio yetu ni kwamba vijiji vyote vya Mkoa wa Morogoro ikifika mwezi Juni mwaka huu viwe vimepatiwa umeme.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile mkakati wetu ni kuhakikisha kwamba tupo katika hatua ya mwisho ya kupeleka umeme kwenye vitongoji 15 vya kila jimbo la nchi yetu na matarajio yetu ni kwamba kazi hii itakamilika, uratibu wa kazi hii utakamilika hivi karibuni na tutaweza kuanza kufanya kazi hiyo.

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, lini Kata za Tchenzema, Lingali, Kikeo na Lwale katika Tarafa ya Mgeta - Morogoro zitapatiwa umeme?

Supplementary Question 2

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Ndani ya Halmashauri ya Mji wa Njombe Kata ya Kambarage kuna mitaa miwili ya Pemba na Unguja mpaka leo haina umeme: Ni lini mitaa hiyo itapata umeme? (Makofi)

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII K.n.y. WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deodatus Mwanyika, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itahakikisha kwamba vijiji vyote ambavyo havina umeme, kufika mwezi Juni vinapata umeme na vile vile kufika Juni kazi ya kupeleka umeme kwenye vitongoji vyote nchini, vile 15 kama nilivyosema awali, itakuwa imefanyika.

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, lini Kata za Tchenzema, Lingali, Kikeo na Lwale katika Tarafa ya Mgeta - Morogoro zitapatiwa umeme?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Ni lini Serikali itapeleka umeme katika Kata za Mwamashele, Lagana pamoja na Mwasubi? (Makofi)

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII K.n.y. WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Mnzava, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, makusudio yetu ni kuhakikisha kwamba mikataba yote ya ukandarasi wa kupeleka umeme kwenye vijiji vyetu, ile mikataba iliyowahi kufika mwezi Juni mwaka huu 2024, umeme utakuwa umepatikana. Mikataba ambayo imechelewa tutasogea mbele kidogo ikiwezekana kufika mwishoni mwa mwaka huu wa fedha (2023/2024). (Makofi)

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, lini Kata za Tchenzema, Lingali, Kikeo na Lwale katika Tarafa ya Mgeta - Morogoro zitapatiwa umeme?

Supplementary Question 4

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Ni lini Serikali itatekeleza mpango wake wa peri urban kupeleka umeme katika mitaa yenye sura za vijiji katika miji yetu ikiwepo katika Manispaa ya Iringa Mtaa wa Ugere, Mosi, Msisina na Mtalagala.

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII K.n.y. WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jesca Msambatavangu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ina mpango wa kupeleka umeme kwenye maeneo ya miji yenye sura za vijiji (peri urban) na kazi hiyo inaendelea kwa sasa. Nimwombe Mheshimiwa Mbunge awe na Subira, kazi hii itakamilika, maeneo haya yatapatiwa umeme.