Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 11 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 177 2024-02-13

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: -

Je, lini Kata za Tchenzema, Lingali, Kikeo na Lwale katika Tarafa ya Mgeta - Morogoro zitapatiwa umeme?

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII K.n.y. WAZIRI WA NISHATI alijibu:

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Christine Gabriel Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaendelea kutekeleza mradi wa kupeleka umeme vijijini katika Mkoa wa Morogoro hususan Tarafa ya Mgeta ambapo mradi unahusisha kusambaza umeme katika Kata za Tahenzewa, Langala, Kikea na Kwale. Mkandarasi anayetekeleza mradi huo katika Tarafa ya Mgeta amekamilisha kazi ya mradi katika Kata ya Tahenzewa katika vijiji vya Tahenzewa na Kibuko na Kata ya Langala, Kijiji cha Pinde.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa Mkandarasi anaendelea na kazi katika Kata ya Tahenzewa, vijiji vya Bumu, Lusungi, Mwarazi na Kata ya Kikea, vijiji vya Lukunguni, Kododo, Chohelo, Mhale, Kikeo na Ng’owo. Utekelezaji wa mradi katika Tarafa ya Mgeta unatarajia kukamilika mwezi Juni, 2024.