Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Charles Muguta Kajege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. CHARLES M. KAJEGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha majengo ya shule na zahanati ambayo yalijengwa kwa nguvu za wananchi katika Jimbo la Mwibara?

Supplementary Question 1

MHE. CHARLES M. KAJENGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize swali moja na nasema ni ombi; kwanza nachukua fursa hii kuipongeza Serikali kwa kazi nzuri sana ambayo inafanyika katika jimbo langu. Naomba Mheshimiwa Waziri anihakikishie kwamba baada ya Bunge hili tutaongozana naye tuweze kwenda Mwibara ili tukatembelee shule za msingi na zahanati husika.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Charles Muguta Kajenge, Mbunge wa Jimbo la Mwibara kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze sana Mheshimiwa Kajege kwa kazi kubwa anayofanya kuhakikisha wananchi wa Jimbo la Mwibara lakini tupokee shukrani nyingi na pongezi zake kwa Serikali yetu inayoongozwa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan na nimuhakikishie kwamba tutaendelea kutekeleza miradi hii kwa mnufaa ya wananchi wa Mwibara, lakini nikuhakikishie kwamba niko tayari tuambatane pamoja baada ya Bunge hili kwenda Mwibara kupita vituo, lakini pia na miradi mingine ya Serikali. Ahsante.

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CHARLES M. KAJEGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha majengo ya shule na zahanati ambayo yalijengwa kwa nguvu za wananchi katika Jimbo la Mwibara?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi; kwa kuwa Serikali imeamasisha wananchi kujenga zahanati katika kila kata na vijiji na maboma mengi hayajakamilika, je, nini kauli ya Serikali kukamilisha maboma hayo katika Halmashauri ya Shinyanga?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Christine Mnzava, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Serikali ilihamasisha wananchi kwa nia njema ya kuhakikisha kwamba wananchi wanapata zahanati na vituo vya afya katika maeneo ya kimkakati na mpango wa Serikali ni kukamilisha zahanati na maboma ya vituo hivyo katika maeneo ya kimkakati kwa maana ya kata za kimakakati na tarafa za kimkakati, siyo kila kata au siyo kila kijiji na kazi hiyo imefanyika sana kwa mfano katika mwaka mmoja maboma ya zahanati 954 yamekamilishwa, mwaka ujao Serikali imetenga bilioni 15 kwa ajili ya kukamilisha maboma 300 ya zahanati, kwa hivyo kazi hii itaendelea kufanyika.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.