Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 43 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 377 2022-06-13

Name

Charles Muguta Kajege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. CHARLES M. KAJEGE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakamilisha majengo ya shule na zahanati ambayo yalijengwa kwa nguvu za wananchi katika Jimbo la Mwibara?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Charles Muguta Kajege, Mbunge wa Jimbo la Mwibara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali imetenga shilingi milioni 287.5 kwa ajili ya ukamilishaji wa vyumba vya madarasa 14 katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda. Aidha, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali imetenga shilingi milioni 240 kwa ajili ya kukamilisha vyumba vya madarasa 14 katika Jimbo la Mwibara pamoja na ukamilishaji wa maabara tatu za kemia, baiolojia na fizikia.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeendelea kutoa fedha kwa ajili ya kukamilisha maboma ya zahanati. Katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali imekwisha peleka kwenye Jimbo la Mwibara shilingi milioni 100 kwa ajili ya kukamilisha maboma mawili ya zahanati za Sozia na Ragata. Aidha, katika mwaka wa fedha 2022/23 shilingi milioni 88 imetengwa kwa ajili ya ujenzi wa Zahanati ya Nyamitwebiri.