Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka mtaalam wa X–Ray katika Hospitali ya Wilaya ya Meatu?

Supplementary Question 1

MHE. MINZA S. MJIKA: Mheshimiwa Spika, ahsante nashukuru na ninashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali kweli Waziri amekuwa akinipa ushirikiano sana.

Lakini nilitaka nijue sasa ni lini mtaalam huyo ataletwa kwa sababu tatizo hili limekuwa ni la muda mrefu sana leo Wilaya ya Meatu hospitali ina zaidi ya miaka 30 lakini hatujawahi kupata mtaalam wa kudumu wa X-ray, ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Minza Simon Mjika, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Minza amekuwa akifuatilia sana sana kwa kushirikiana na Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Meatu kupata mtumishi kwa ajili ya huduma za X-ray kwenye hospitali ya Meatu na nimuhakikishie kwamba katika ajira hizi ambazo tunakamilisha na mpango ni kuanzia Julai watumishi wetu watapelekwa vituoni tutapeleka mtaalam wa X-ray kwenye hospitali hii ya Meatu, ahsante. (Makofi)

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka mtaalam wa X–Ray katika Hospitali ya Wilaya ya Meatu?

Supplementary Question 2

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza siku ya leo.

Mheshimiwa Spika, mwezi Oktoba mwaka jana Mheshimiwa Waziri Mkuu alitembelea katika Jimbo la Kilwa Kaskazini na alifika katika hospitali ya Kipatimu na akakuta kuna changamoto kubwa ya mtumishi wa X-ray baada ya kuwa X-ray ilinunuliwa miaka zaidi ya minne kabla ya mwaka jana ikiwa haitumiki kutokana na kukosa mtumishi wa X-ray.

Mheshimiwa Spika, swali langu ni kwamba mtumishi huyu aliletwa akakaa miezi sita lakini juzi juzi hapa ameondolewa, nataka kujua je, Serikali ina mpango gani wa kumrejesha yule mtumishi ambaye ameondolewa juzi juzi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Francis Kumba Ndulane, Mbunge wa Jimbo la Kilwa Kaskazini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba tulipeleka mtumishi Hospitali ya Kipatimu lakini kwa sababu za kiutumishi amehamishwa, lakini kwenye ajira hizi ambazo watumishi watapelekwa mwezi Julai tayari ameshapangwa mtumishi wa X-ray kwenye Hospitali ya Kipatimu, ahsante.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka mtaalam wa X–Ray katika Hospitali ya Wilaya ya Meatu?

Supplementary Question 3

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Pamoja na uhaba wa watumishi/wataalam wa hivyo vifaa tiba lakini pia ma-engineer au mafundi wa kutengeneza hivyo vifaa tiba pindi inapoharibika inakuwa ni changamoto kubwa sana.

Je, katika ajira zilizoko mnazingatia pia na wataalam hawa ili inapopata breakdown yoyote basi inatengenezwa kwa wakati?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cecilia Paresso, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Ni kweli kwamba tumekuwa na changamoto ya upungufu wa wataalam wa vipimo kwa maana diagnostic issues ikiwemo X-ray na ultrasound, lakini Serikali kwanza tumeweka mpango mkakati wa kuwafanyia mafunzo kazini wataalam zaidi ya 300 ambao watakwenda ku-cover mapengo kwenye vituo vya afya na hospitali ambazo zinajengwa ili yale majengo yaliyojengwa na vifaa tiba ambavyo vinakwenda vianze kutumika mapema iwezekanavyo.

Lakini pili tuna wataalam wa ufundi kwa maana ya biomedical engineers katika halmashauri zetu na katika ajira hizi pia wataajiri wataalam hao, ahsante.

Name

Charles Muguta Kajege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka mtaalam wa X–Ray katika Hospitali ya Wilaya ya Meatu?

Supplementary Question 4

MHE. CHARLES M. KAJEGE: Mheshimiwa Spika, ahsante, vituo vya afya vya Kasaunga, Kisorya na Kasuguti bado havina mashine za X-ray; je, ni lini vituo hivi vitapata hizo mashine?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Charles Kajege, Mbunge wa Jimbo la Mwibara kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kupitia mpango wa UVIKO-19 Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ametoa fedha kwa ajilli ya kununua digital X-ray 65 kwa ajili ya halmashauri zetu, lakini kwa sababu tunakwenda kununua kwa utaratibu wa kushirikiana na wenzetu wa UNICEF zinaweza zikafika zaidi ya 80, 90.

Kwa hiyo vituo vingi vile ambavyo vinahitaji X-ray vitapata, lakini kwa maana ya hospitali za wilaya kama kipaumbele na baadaye tutakuja kwenye vituo hivyo na tuta-consider pia vituo vya Mwibara, ahsante.

Name

Yustina Arcadius Rahhi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka mtaalam wa X–Ray katika Hospitali ya Wilaya ya Meatu?

Supplementary Question 5

MHE. YUSTINA A. RAHHI: Mheshimiwa Spika, na mimi nina swali la nyongeza; hospitali ya halmashauri ya Mji wa Mbulu X-ray machine mbovu, kwa hiyo kufanya watu hawa kuhangaika kwenda kwenye vituo vya afya. Je, Serikali inapeleka lini X-ray machine katika Hospitali ya Mji wa Mbulu?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Yustina, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika X-ray ambazo zitaletwa kipaumbele ni hospitali za halmashauri, kwa hiyo tunachukua hoja ya hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Mbulu ili tuone kama ile X-ray haiwezi kufanyakazi basi tuhakikishe katika awamu hii tunapeleka X-ray pale wananchi wapate huduma, ahsante.

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka mtaalam wa X–Ray katika Hospitali ya Wilaya ya Meatu?

Supplementary Question 6

MHE. DKT. MATHAYO D. MATHAYO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi hii niweze kuuliza swali la nyongeza kwa Jimbo la Same Magharibi.

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya Hedaru na Kituo cha Afya cha Kisiwani, ni vituo ambavyo vinahudumia watu wengi sana lakini vina upungufu wa vifaa tiba. Je, ni lini Serikali itahakikisha kwamba Kituo cha Afya Hedaru na kile cha Kisiwani kinapata vifaa tiba vya kutosha?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Mathayo David Mathayo, Mbunge wa Jimbo la Same Magharibi kama ifuatavyo: -

Katika bajeti ya mwaka ujao wa fedha 2022/2023 Serikali imetenga shilingi bilioni 69.95 kwa ajili ya kununua vifaa tiba kwenye hospitali za halmashauri zilizokamilika na vituo vya afya vilivyokamilika vya awamu ya kwanza.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo kama vituo hivi vipo awamu ya kwanza nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba vitapata vifaa tiba lakini kama viko awamu ya pili na ya tatu basi vitapata awamu itakayofuata, ahsante.