Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Juma Usonge Hamad

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chaani

Primary Question

MHE. JUMA USONGE HAMAD aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kutoa matibabu bure kwa maradhi yasiyoambukiza kama kisukari, pressure na shinikizo la damu?

Supplementary Question 1

MHE. JUMA USONGE HAMAD: Mheshimiwa Spika, ahsante sana; kwa kuwa utaratibu wa kutoa msamaha kwa wazee umekuwa na mlolongo mrefu, lakini wazee hao wanakatishwa tamaa wanapopata hizo huduma.

Je, ni ipi kauli ya Serikali ya kupunguza mlolongo huo?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, toka Bunge hili kuanza tumekuwa tumesikia sana hizi kauli za kusema kwamba inakuja Bima ya Afya kwa Wote.

Je, ni nili hasa Serikali italeta Muswada wa Bima ya Bure kwa Wote? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, moja la kwanza; suala la ukiritimba kwenye msamaha kwa wazee na kuwahudumia wazee. Kwanza nitumie fursa hii kutoa agizo kwa Waganga wote Wakuu wa Mikoa na Waganga Wakuu wa Wilaya kwamba suala la tiba kwa wazee siyo tu kwamba ni bure lakini vilevile wanatakiwa wawe na dirisha lao. Kwa hiyo, hatutegemei tena kusikia haya malalamiko ya kwamba wazee wanapata mlolongo mrefu wa kupata tiba. Lakini Waganga Wakuu wa Wilaya wahakikishe vilevile wazee wamepata vile vitambulisho vyao.

Mheshimiwa Spika, la pili, kwamba ni lini sasa Muswada huu utakamilika, Mheshimiwa Mbunge hili nisije nikalidanganya Bunge ninachoomba tutalishughulikia na mapema sana tunaweza tukaja kukuambia ni nini kitakachofanyika kabla Bunge hili halijaisha. Lakini kwa sasa ukinipa tarehe specific inaihusu organ mbalimbali za Serikali ili hilo liweze kuja hapa Bungeni, naomba nilifuatilie kwa uhakika zaidi. (Makofi)