Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 41 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 366 2022-06-09

Name

Juma Usonge Hamad

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chaani

Primary Question

MHE. JUMA USONGE HAMAD aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kutoa matibabu bure kwa maradhi yasiyoambukiza kama kisukari, pressure na shinikizo la damu?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya naomba kujibu swali la Mheshimiwa Juma Usonge Hamad, Mbunge wa Jimbo la Chaani kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba matibabu ya magonjwa yasiyoambukiza yana gharama kubwa na yanahitaji tiba wakati wote. Serikali imekuwa ikitoa msamaha wa matibabu kwa wagonjwa ambao wamethibitika hawana uwezo wa kugharamikia matibabu hayo kwa mujibu wa Sheria ya Afya. Hata hivyo, Serikali ipo katika hatua ya mwisho za ukamilishaji wa Muswada wa Bima ya Afya kwa wote ambao utawezesha wananchi wote kupata huduma za afya katika Vituo vya Afya nchini, ahsante. (Makofi)