Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga daraja katika eneo la Jangwani barabara ya Morogoro Jijini Dar es Salaam ili kuondoa usumbufu na adha wanazopata wananchi hasa wakati wa mvua?

Supplementary Question 1

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri; sote tunatambua umuhimu wa eneo hili la Jangwani barabara ya Morogoro kama kiunganishi.

Mheshimiwa Spika, nina maswali mawili (a) na (b); kwa sababu mvua zitaendelea kunyesha, tope, takataka, magugu, mafuriko yataendelea kuwepo na usumbufu upo kwa watumiaji wa pale.

Je, Serikali ina mpango gani wa dharura wakati tukisubiri huo mpango ambao utaratibu wake unaonekana kuchukua muda mrefu?

Swali la pili, hapo siku za nyuma Serikali ilitueleza mpango mzuri wa kuendeleza eneo lile la Jangwani ikiwemo kuunganisha na kupitia pembezoni mwa mto mpaka Salender Bridge pamoja na kuwekwa viwokwe. Naomba kuuliza Serikali mpango ule mzuri wa kuendeleza eneo lile la Jangwani umefikia wapi? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Asha Abdullah Juma, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tuna mpango wa dharura ambao unatumika kuhakikisha kwamba daraja lile linapitika na ndiyo maana utaona pamoja na kwamba mvua zinanyesha, lakini bado daraja linaendelea kupitika. Tumemuweka mkandarasi kwa lile daraja ambaye kila baada ya mvua kunyesha anaondoa mchanga, udongo na taka ngumu mita 500 juu na mita 500 chini ili kuruhusu maji yaweze kupita na changamoto hii inasababisha tu na watu kufnayakazi karibu na mto ule. Kwa hiyo, nitoe pia rai kwa wanaofanyakazi wasifanye kazi karibu na kingo za mto ambazo zinasababisha kushindwa kupitika kwa maji kwenye daraja.

Mheshimiwa Spika, suala la pili alilouliza mpango wa kuendeleza Bonde la Jangwani ni kweli upo kupitia mpango wa DMDP, lakini pia nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wa Dar es Salaam ambao walikaa na Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, TAMISEMI pamoja Hazina kwamba Serikali imeamua kwamba itajenga flyover ambayo itakuwa inaunganisha makutano ya fire na makutano ya Magomeni, ahsante.

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga daraja katika eneo la Jangwani barabara ya Morogoro Jijini Dar es Salaam ili kuondoa usumbufu na adha wanazopata wananchi hasa wakati wa mvua?

Supplementary Question 2

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi.

Kutokana na mvua nyingi zilizonyesha mwaka jana kuna madaraja matatu ndani ya Wilaya ya Ludewa ambayo yapo chini ya TANROADS yaliharibika. Eneo la Muhoro, Nyapandi na Ludewa Vijijini, je, lini Serikali itajenga madaraja ya kudumu?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Neema Mgaya, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, nataka nimuhakikishie Mbunge kwamba baada ya changamoto ya hayo madaraja bahati nzuri mimi nimekwenda na nimefika na tumefanya ukarabati na tunachokifanya sasa hivi katika bajeti hii ni kuagiza madaraja mengi ya vyuma ambayo yatatumika pale panapotekea changamoto ili kuweza kuokoa na kufanya matengenezo ya haraka ili kurudisha mawasiliano, ahsante.

Name

Agnesta Lambert Kaiza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga daraja katika eneo la Jangwani barabara ya Morogoro Jijini Dar es Salaam ili kuondoa usumbufu na adha wanazopata wananchi hasa wakati wa mvua?

Supplementary Question 3

MHE. AGNESTA L. KAIZA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili nami niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Kwa kuwa eneo la makutano ya Mkwajuni, Kinondoni na Mto Msimbazi hukumbwa na mafuriko kipindi cha mvua kama ilivyo Jangwani na hivyo kusababisha adha kubwa sana kwa wananchi wa makazi hayo.

Mheshimiwa Spika, swali langu; je, Serikali ipo tayari kujenga daraja la kudumu ili kuondoa kero hii kwa wananchi ambayo imedumu kwa muda mrefu? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Lambert Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, daraja alilotaja pia ni sehemu ya Bonde la Jangwani ambalo litafanywa pamoja kwenye Mpango wa DMDP ili kuboresha usafiri katika eneo hilo. Ahsante.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga daraja katika eneo la Jangwani barabara ya Morogoro Jijini Dar es Salaam ili kuondoa usumbufu na adha wanazopata wananchi hasa wakati wa mvua?

Supplementary Question 4

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, ahsante; je, ni lini Serikali itajenga daraja linalounganisha Kalya na Ilagala katika Mto Malagarasi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Josephine Genzabuke, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, daraja hili tunaita daraja la Malagarasi Chini na daraja hili pana kivuko kwa hiyo kuanzia mwaka huu wa fedha na mwaka unaokuja tunaendelea na tumetenga fedha ambapo tutakamilisha kufanya usanifu kwa ajili ya maandalizi ya kujenga daraja la kudumua kuunganisha Kigoma na eneo Kalya, ahsante.

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga daraja katika eneo la Jangwani barabara ya Morogoro Jijini Dar es Salaam ili kuondoa usumbufu na adha wanazopata wananchi hasa wakati wa mvua?

Supplementary Question 5

MHE. DEUS C. SANGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana; Daraja la Mto Mlokola ambalo lipo ndani ya Kata ya Mlokola ni daraja ambao lina hali mbaya sana na juzi tu limesababisha ajali kubwa iliyogharimu maisha ya wananchi wangu ndani ya Jimbo la Kwela.

Je, ni lini Serikali itatengeneza daraja hilo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante na napenda kujibu swali la Mheshimiwa Deus Sangu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba nimuagize Meneja wa TANROADS aende kwenye daraja hili akafanye tathmini ili tujue changamoto na tuone gharama ili tuweze kurejesha mawasiliano ya daraja hili ambalo Mheshimiwa Mbunge amelitaja, ahsante. (Makofi)

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga daraja katika eneo la Jangwani barabara ya Morogoro Jijini Dar es Salaam ili kuondoa usumbufu na adha wanazopata wananchi hasa wakati wa mvua?

Supplementary Question 6

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi, barabara ya Mafinga kwende Mgololo eneo la Itulavano, daraja lililopo ni jembamba sana na barabara hii inatumika na malori yanayobeba mazao ya misitu.

Je, Serikali ipo tayari kulirekebisha na kulijenga daraja hili ili liwe pana kumudu magari hayo mazito? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cosato Chumi, Mbunge wa Mafinga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli hii barabara aliyoitaja ndiyo barabara ambayo kwa asilimia kubwa inapitisha mbao sehemu kubwa ambazo tunaziona, lakini barabara aliyoitaja pamoja na daraja iko kwenye mpango wa kuanza kuijenga kwa kiwango cha lami ikiwa ni pamoja na kulijenga hilo daraja ambalo litaendana na barabara hiyo, ahsante. (Makofi)

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga daraja katika eneo la Jangwani barabara ya Morogoro Jijini Dar es Salaam ili kuondoa usumbufu na adha wanazopata wananchi hasa wakati wa mvua?

Supplementary Question 7

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Kwa kuwa ujenzi wa madaraja haya ya juu (flyovers) yamekuwa yana lengo la kupunguza foleni, lakini baada ya ujenzi wenyewe tu kunakuwa na kuwekwa matuta sasa kwenye barabara ambayo inakwenda ku-distort au kuharibu ile dhima ya kujenga zile flyover.

Je, ni ipi kauli ya Serikali juu ya mkanganyiko huu? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mtemvu, Mbunge wa Kibamba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli lengo la flyover ni kupunguza foleni na hili alilolisema wakati fulani inakuwa ni kwa ajili ya usalama kwamba tuweke matuta ili kupunguza ajali. Kwa hiyo, tutazingatia kuona kama hakuna ulazima wa kuweka hayo matuta tutayaondoa, lakini tukizingatia sana kwamba usalama wa wale watumiaji wa hizo barabara, ahsante.

Name

Muharami Shabani Mkenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga daraja katika eneo la Jangwani barabara ya Morogoro Jijini Dar es Salaam ili kuondoa usumbufu na adha wanazopata wananchi hasa wakati wa mvua?

Supplementary Question 8

MHE. MUHARAMI S. MKENGE: Mheshimiwa Spika, ni lini Serikali itajenga daraja linalounganisha kati ya Mbweni na Mapinga, Bagamoyo ili kupunguza foleni? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Kibaha kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, daraja alilolitaja pia ni barabara ambayo ipo kwenye bajeti ya mwaka huu kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami na tunapojenga barabara hizo ni pamoja na madaraja yanayohusika kwenye hizo barabara, ahsante.