Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 41 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 365 2022-06-09

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga daraja katika eneo la Jangwani barabara ya Morogoro Jijini Dar es Salaam ili kuondoa usumbufu na adha wanazopata wananchi hasa wakati wa mvua?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Asha Abdullah Juma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi wa daraja jipya la Jangwani chini ya ufadhili wa Benki ya Dunia ili kutatua tatizo la mafuriko imekamilika na Serikali inaendelea na mazungumzo na Benki ya Dunia ili kupata fedha kwa ajili ya ujenzi wa daraja hilo. Ahsante.