Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: - Je, ni lini Mradi wa Maji wa Ikozi uliopo Sumbawanga Vijijini utakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawilli ya nyongeza.

Swali la kwanza; Serikali ina mpango gani sasa wa kuwalipa fidia wananchi ambao walikuwa wanaishi katika eneo lile na walikuwa wanalima mashamba yao?

Swali la pili, shida iliyoko Ikozi ni sawa na shida iliyoko Mpui kata ambazo zinakaribiana, Serikali sasa ina mpango gani wa kukamilisha mradi ulioko Mpui pale ambao mradi upo lakini wananchi hawapati maji?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Bupe Mwakang’ata kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali ina mpango gani wa kulipa fidia, tayari Serikali kupitia Wizara ya Maji kwa maeneo ambayo miradi inapita tumeshaanza malipo na mradi wa eneo hili pia watafikiwa hivi punde. Kata zinazokaribiana hiyo Kata ya Mkuyu na yenyewe pia kuna mradi, mradi huu sasa hivi tunaendelea kuufuatilia kwa karibu sana kuhakikisha dhima ya Serikali kumtua mama ndoo kichwani inakwenda kutekelezeka hata kwa wananchi watokao Mkuyu.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: - Je, ni lini Mradi wa Maji wa Ikozi uliopo Sumbawanga Vijijini utakamilika?

Supplementary Question 2

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri swali kwamba tunampongeza Mheshimiwa Rais kwa kazi nzuri ambayo ameifanya jana kwa miji 28 kupata mradi wa maji na kwa kweli kwa nchi nzima kuna mabadiliko makubwa sana ya maji hata Tarime kuna mabadiliko makubwa sana.

Sasa nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba nilikuuliza swali hapo ukasema Tarime itapata maji katika miji ile 28, lakini kwenye hii list ya jana Tarime haimo; nini kauli ya Serikali juu ya watu wa Tarime ili waweze kusubiri maji? Ahsante.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Waitara kama ifuatavyo: -

Tarime imo Rorya, Tarime ipo kwenye mradi wa miji 28; vuta subira wakati wa utekelezaji utakapoanza utashuhudia kwamba Tarime imo. (Makofi)