Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 39 Water and Irrigation Wizara ya Maji 349 2022-06-07

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: -

Je, ni lini Mradi wa Maji wa Ikozi uliopo Sumbawanga Vijijini utakamilika?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bupe Nelson Mwakang’ata, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali imeendelea na utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Bwawa la Ikozi unaohudumia Viijiji vya Ikozi, Kazwila, Chituo na Tentula vya Kata ya Ikozi, Wilaya ya Sumbawanga Vijijini. Mradi huo unahusisha ujenzi wa bwawa, ulazaji wa bomba kuu umbali wa kilometa 1.2, nyumba ya mtambo, ununuzi na ufungaji wa pump za kusukuma maji na ujenzi wa mfumo wa kusafisha na kutibu maji. Utekelezaji wa mradi utakamilika katika mwaka wa fedha 2022/2023.