Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza: - Je, ni lini wananchi wa Jimbo la Nkenge ambao hawajapata Vitambulisho vya Taifa au Namba za Usajili watatambuliwa kama raia wenye haki na kupatiwa vitambulisho hivyo?

Supplementary Question 1

MHE. FLORENT L. KYOMBO: Mheshimiwa Spika, nishukuru kwa nafasi, na naipongeza Serikali kwa majibu mazuri, lakini ndani ya muda mfupi wameweza kutengeneza vitambulisho. Naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; Wilaya ya Misenyi kama alivyosema Mheshimiwa Naibu Waziri, imetengeneza vitambulisho 24,000 lakini mpaka sasa ni vitambulisho 5,000 vimegawiwa kwa wananchi. Shida kubwa ni kwamba wananchi wanatakiwa kuhakikiwa kwa mara nyingine, hii imekuwa ni kero kubwa kwa wananchi wa Wilaya ya Misenyi na hivyo wananchi kuona kwa kweli kuona kwamba sio sahihi kuhakikiwa mara ya pili.

Je, ni nini tamko la Serikali kuhusiana na usumbufu huo?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, sasa kuna baadhi ya wananchi ambao walikuwa hawajafikiwa kwa ajili ya kujaza fomu kwa ajili ya kupata vitambulisho ikiwa ni pamoja na wale ambao wamefikisha umri wa miaka 18 ambao wametiza sasa vigezo sasa vya kupata vitambulisho.

Je, ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha na wananchi hao wanafikiwa kwa ajili ya kupata vitambulisho? Ahsante.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kyombo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusu idadi ndogo ya wananchi waliogaiwa vitambulisho 5,000 tu kati ya wananchi 24,694 ambao vitambulisho vyao vimetoka, nitoe tu maelekezo kwa wenzetu wa NIDA Mkoa wa Kagera na hususan Wilaya ya Misenyi kwamba wakati wanawahakiki mwanzo mpaka vitambulisho vinatoka bila shaka walikuwa wamejiridhisha. Hata hivyo, pale ambapo kuna mashaka kwamba huenda wanaokwenda kutoa vitambulisho siyo raia wa Tanzania wana haki ya kufanya uhakiki mara ya pili; lakini uhakiki huo usiwe sehemu ya usumbufu kwa wananchi kwa sababu haieleweki kwa nini wananchi 5,000 pekee kati ya 24,000 ndiyo wapate. Kwa hiyo, waharakishe uhakiki huo ili wanaostahili kweli waweze kupewa vitambulisho vyao.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali la pili la mkakati wa Serikali, tumelijibu kwa nyakati tofauti kwamba tulikuwa na changamoto ya kimkataba kati ya Serikali na Mkandarasi, lakini changamoto hiyo imemalizwa na mkataba umeuhishwa mwezi Machi, 2022; kwa hiyo, wakati wowote kuanzia sasa vitambulisho vingine vitazalishwa na watu wengine ambao wamefikisha miaka 18 wataendelea kutambuliwa kwa madhumuni ya kupewa vitambulisho vyao. Nashukuru.

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza: - Je, ni lini wananchi wa Jimbo la Nkenge ambao hawajapata Vitambulisho vya Taifa au Namba za Usajili watatambuliwa kama raia wenye haki na kupatiwa vitambulisho hivyo?

Supplementary Question 2

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa fursa ya kuweza kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kumekuwa kuna wanafunzi wa Shule za Sekondari ambao wamekuwa wakimaliza shule na wanazaidi ya miaka 18. Je, nini mkakati wa Serikali kutoa elimu katika shule mbalimbali ili wanafunzi wanapomaliza waliozaidi ya miaka 18 waweze kupata vitambulisho?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Fatma Toufiq, Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba baadhi ya wanafunzi huitimu masomo yao wakiwa na zaidi ya miaka 18 na wanafunzi wa aina hii wana haki ya kupewa vitambulisho. Kwa hiyo, pengine tutashirikiana na Wizara ya Elimu na Wizara ya TAMISEMI ili elimu ya uraia ikiwa ni pamoja na nafasi ya kuwa na vitambulisho kutolewa mashuleni, lakini wanafunzi hawa ni sehemu ya jamii kule ambako elimu inatolewa kwenye jamii kwa ujumla wake kupitia redio, televisheni na kadhalika wanaweza pia wakapata elimu hiyo. Kwa hiyo, nadhani halitakuwa tatizo kubwa sana litatekelezwa. Nashukuru sana.

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza: - Je, ni lini wananchi wa Jimbo la Nkenge ambao hawajapata Vitambulisho vya Taifa au Namba za Usajili watatambuliwa kama raia wenye haki na kupatiwa vitambulisho hivyo?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Spika, nashukuru, wananchi wanaoishi Visiwa vidogo vidogo Jimboni Ukerewe wanalazimika kusafiri kwenda Makao Makuu ya Wilaya kufuatilia vitambulisho vya NIDA jambo linalopelekea usumbufu na gharama kubwa.

Nini mkakati wa Serikali kuwapelekea huduma lakini wakati huo huo ikiwaondolewa usumbufu wa wananchi hao? Nashukuru.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mkundi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ili kuwapunguzia usumbufu hawa wananchi wanaokaa mbali na makao makuu wakiwepo hawa wa visiwani, vitambulisho hivi vimepelekwa mpaka ngazi ya Kata ili maofisa wetu kwenye ngazi ile aweze kuwagawia wananchi wao, nadhani kwa kufanya hivyo tutakuwa tumepunguza usumbufu wa wananchi. Naomba niwaelekeze wenzetu wa Ukerewe kama lipo tatizo la kuwataka wananchi wote wasafiri kwenda Nansio warekebishe ili vitambulisho hivi wavipate kwenye Makao Makuu ya Kata zao. Nashukuru.

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza: - Je, ni lini wananchi wa Jimbo la Nkenge ambao hawajapata Vitambulisho vya Taifa au Namba za Usajili watatambuliwa kama raia wenye haki na kupatiwa vitambulisho hivyo?

Supplementary Question 4

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa wananchi wengi wanapata tatizo na eneo hili la uhakiki kwa ajili ya kupata hivyo Vitambulisho vya Taifa. Sijui Serikali inasemaje kuhusu muda hasa ni muda gani ambao uhakiki unachuku ili wananchi waweze kupata vitambulisho vyao?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, uhakiki hautakiwi kuchukua muda mrefu sana, lakini tunafanya uhakiki ili tujiridhishe kwamba wanaopewa vitambulisho hivi ni raia wa Tanzania. Kwa hiyo, itakapotokea taarifa yoyote hasa wananchi wakatia mashaka juu ya mtu aliyetambuliwa inabidi tufanye uhakiki kujiridhisha.

Sasa juu ya muda gani itategemea pale itakapokamilisha, lakini aombe maafisa wetu wasichukue muda mrefu kwa sababu wanapaswa kushirikiana na vyombo vingine vikiwa Kamati za Usalama za Wilaya na Idara za Uhamiaji ili kujiridhisha na kumpa jibu yule ambaye anatafuta kitambulisho. Nashukuru.