Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 39 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 345 2022-06-07

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza: -

Je, ni lini wananchi wa Jimbo la Nkenge ambao hawajapata Vitambulisho vya Taifa au Namba za Usajili watatambuliwa kama raia wenye haki na kupatiwa vitambulisho hivyo?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Florent Laurent Kyombo, Mbunge wa Jimbo la Nkenge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali ina jukumu la kuhakikisha upatikanaji wa Vitambulisho vya Taifa kwa wananchi ikiwemo wananchi wa Jimbo la Nkenge. Katika Mkoa wa Kagera jumla ya wananchi 1,009,653 wamesajiliwa na kutambuliwa baada ya maombi yao kuhakikiwa. Jumla ya vitambulisho 310,847 vimezalishwa kwa ajili ya wananchi wa mkoa huo. Katika Wilaya ya Misenyi inayojumuisha jimbo la Nkenge wananchi 85,439 wamesajiliwa na kutambuliwa na jumla ya wananchi 32,235 wamepatiwa Namba za Utambulisho ambazo wanazitumia katika kupata huduma mbalimbali. Aidha, vitambulisho 24,694 vimezalishwa na kugaiwa kwa wananchi wa Wilaya hiyo. Nashukuru.