Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kuipandisha hadhi Zahanati ya Kijiji cha Sojo ili kiwe Kituo cha Afya na kuweza kuhudumia wananchi na watumishi wa Mradi wa Bomba la Mafuta?

Supplementary Question 1

MHE. SELEMANI J. ZEDI: Mheshimiwa Spika, ahsante, nashukuru sana kwa jibu zuri sana lililotolewa na Mheshimiwa Waziri na nichukue nafasi hii kuipongeza Serikali ya Awamu Sita, chini ya Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea na kutupatia shilingi milioni 500 kwa ajili ya kujenga Kituo cha Afya pale Sojo Igusule.

Mheshimiwa Spika, sasa swali langu ni kwamba Mheshimiwa Waziri, utakuwa tayari baada ya Bunge hili la bajeti uongozane na mimi kwenda Kijiji cha Sojo ili wananchi wa Sojo Igusule wakakushukuru kwa kutupatia shilingi milioni 500 za kujenga kituo cha afya ambacho tulikuwa tunakihitaji sana?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Selemani Jumanne Zedi, Mbunge wa Jimbo la Bukene kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, nimpongeze sana Mheshimiwa Zedi amekuwa akifuatilia sana juu ya ujenzi wa kituo hiki cha afya na Serikali sikivu ya Awamu wa Sita, inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Mama Samia Suluhu Hassan, imewasikia wananchi wa Jimbo la Bukene, na kituo hicho kitakuja na niko tayari kuongozana nawe kwenda Sojo ili wananchi waweze kumshukuru Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya kutoa fedha kwa ajili ya kituo cha afya hicho. Ahsante. (Makofi)

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kuipandisha hadhi Zahanati ya Kijiji cha Sojo ili kiwe Kituo cha Afya na kuweza kuhudumia wananchi na watumishi wa Mradi wa Bomba la Mafuta?

Supplementary Question 2

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza.

Mchakato wa upandishaji hadhi wa zahanati zetu kwenda vituo vya afya unafanywa na Wizara; je, Wizara haioni sasa mchakato huu mkaziachia Sekretarieti za Mikoa ifanye kazi hiyo kwa vigezo vilevile ili kupunguza huo urasimu?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cecilai Paresso, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, upandishaji hadhi wa zahanti kuwa vituo vya afya au kuwa hospitali za Halmashauri unafanya na Wizara kwa kushirikiana na Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa ambapo Halmashauri wanafanya tathmini kulingana na vigezo, wanawasilisha mikoani kwa RAS na wanawasilisha Wizara ya Afya, lakini pia Ofisi ya Rais – TAMISEMI.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo utaratibu huu ni shirikishi haifanyi Wizara pekee yake ni ngazi zote zinahusika na tutaendelea kufanya hivyo kwa sababu ndiyo maana ya D by D. Ahsante sana.