Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Jasson Samson Rweikiza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa Chuo cha VETA Burugo – Nyakato katika Jimbo la Bukoba Vijijini utakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya swali la nyongeza. Awali napenda niipongeze na kuishukuru Serikali kwa hatua iliyofikia ya ujenzi wa Chuo cha VETA, kizuri, lakini nina swali moja la nyongeza.

Je, mara tutakapoanza kuchukua wanafunzi na kuwaingiza kwenye masomo, wanafunzi hawa wa chuo hiki watapatiwa mikopo ya Serikali ili masomo yaweze kutolewa vizuri? Ahsante.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Rweikiza, Mbunge wa Bukoba Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hivi sasa bado Serikali hatujaanza utaratibu wa kutoa mikopo kwa wanafunzi hawa wa VETA na vyuo vingine vya kati. Kwa hiyo, tunachofanya ni nini sasa kama Serikali? Tunachofanya kama Serikali kwa vyuo hivi vya kati pamoja na VETA, tumejaribu kupeleka ruzuku kwenye maeneo hayo na ndio maana utaona hata ada zake tofauti na vile vyuo vingine vya juu. Ada kwa wanafunzi hawa wa VETA kwa wale wa bweni ni shilingi 120,000 na wale wa kutwa ni shilingi 60,000 ambayo sio thamani halisi ya mafunzo hayo pale, lakini baada ya Serikali kuona umuhimu wa mafunzo haya imeamua kutoa ruzuku.

Kwa hiyo, kwa hivi sasa bado hatujaanza kutoa mikopo. Tunalibeba kama ushauri tuweze kuangalia katika kipindi kijacho kulingana na hali ya upatikanaji wa fedha kama tunaweza tukatoa mikopo katika maeneo haya. Nakushukuru sana.

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa Chuo cha VETA Burugo – Nyakato katika Jimbo la Bukoba Vijijini utakamilika?

Supplementary Question 2

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Kwanza kabisa tunapenda kuishukuru Serikali kwa kutujengea Chuo cha VETA Mkoa wa Rukwa, chuo cha kisasa, chuo kizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali langu ni lini sasa chuo hicho kitafunguliwa na wanafunzi waweze kupata mafunzo? Ahsante.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kulikuwa na mikoa ambayo vyuo vya VETA vya mikoa bado havijakamilika, miongoni mwa mikoa hiyo ni pamoja na Mkoa wa Rukwa na mwingine ni Mkoa wa Njombe, Geita pamoja na Simiyu.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge ukamilishaji wa majengo yale sasa unakamilika. Katika fedha zile za Uviko-19 tulizopata mwaka uliopita tumeweza kupeleka pale zaidi ya bilioni nne kwa ajili ya ukamilishaji wa chuo kile na tunataraji ujenzi ule unaweza ukakamilika katika kipindi hiki kifupi cha mwezi huu wa Juni na mwezi wa Julai, ili basi ifikapo mwezi wa kumi au mwezi Januari mwakani mafunzo pale yaweze kuanza. Nakushukuru sana.

Name

Furaha Ntengo Matondo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa Chuo cha VETA Burugo – Nyakato katika Jimbo la Bukoba Vijijini utakamilika?

Supplementary Question 3

MHE. FURAHA N. MATONDO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa, Jinbo la Buchosa lina watu wanaozidi laki nne, lakini hawana Chuo cha VETA; je, ni lini Serikali itajenga chuo cha VETA katika Halmashauri ya Buchosa ili wananchi wale waweze kupata elimu, lakini pia waweze kujiajiri? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Furaha, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, sera yetu ya elimu na hata katika Ilani ya Chama Cha Mapinduzi inazungumza ujenzi wa Chuo cha VETA katika kila Wilaya nchini. Kwa hiyo, nimuondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge kwamba, tumeanza. Tulianza na Wilaya 25, lakini Wilaya nne nazo vilevile zilikuwa tayari zimeshajengewa katika mwaka ule uliopita wa fedha na sasa hivi Serikali tuko mbioni katika utafutaji wa fedha, ili basi Wilaya zilizobaki karibu Wilaya 70 tuweze kukamilisha ujenzi huu wa vyuo vya VETA katika Wilaya zote nchini. Nakushukuru sana.