Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaipatia ruzuku Bodi ya Maji ya KAVIWASU kwa kuwa imekuwa ikiendeshwa kwa gharama za wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni nini dhamira au msukumo wa Serikali wa kufikiria kuanzisha taasisi moja badala ya kuimarisha taasisi zilizopo na hususan hii taasisi ya KAVIWASU kwa sababu imekuwa ikifanya vizuri zaidi kulinganisha na ile taasisi ya Serikali?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; utozaji wa bei kati ya taasisi hizi mbili hutofautiana na ni ukweli kwamba hiyo taasisi ya Serikali inapata unafuu na bei yake inakuwa nafuu kwa sababu, inapata ruzuku kutoka Serikalini, ilhali ile taasisi iliyoanzishwa na wananchi haipati unafuu wowote na gharama zinabaki palepale. Serikali kwa mara nyingine mpo tayari kuipa ruzuku taasisi hii ya wananchi ili kuunga mkono jitihada za wananchi katika kupata maji katika Mji Mdogo wa Karatu? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Cecilia Paresso, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, lini tutaweka hizi taasisi kuwa moja; mara baada ya taratibu zote za Kiserikali kukamilika tutahakikisha tunafanya hizi taasisi mbili inakuwa moja kama nilivyojibu kwenye jibu langu la msingi.

Mheshimiwa Naibu Spika, utozaji wa bei unatofautiana, chombo ambacho kinasimamiwa na Serikali kinapewa ruzuku na kile cha wananchi hakipewi ruzuku; kitakachofanyika ni kitakuwa chombo kimoja kwa hiyo, ruzuku ya Serikali itaingia na lengo la Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mama mpendwa anayetaka akinamama tuwatue ndoo kichwani, tuhakikishe huduma zinakuwa chini, tutahakikisha bei zinakuwa rafiki kwa wananchi na ruzuku pale inapobidi itakuwa inafika kwa wakati.