Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 37 Water and Irrigation Wizara ya Maji 333 2022-06-03

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaipatia ruzuku Bodi ya Maji ya KAVIWASU kwa kuwa imekuwa ikiendeshwa kwa gharama za wananchi?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante; kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cecilia Daniel Paresso, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa Sheria ya Maji Namba 5 ya mwaka 2019 ya Usambazaji wa Maji na Usafi wa Mazingira kupitia kifungu cha 13(1)(b) vyombo vya watumia maji vinaruhusiwa kutoa huduma za maji kwa wananchi katika maeneo mbalimbali nchini ambapo chombo cha watumia maji cha KAVIWASU kinatoa huduma kwenye baadhi ya maeneo ya mji wa Karatu. Dhamira ya Serikali ni kuhakikisha hakuna changamoto katika utoaji wa huduma ya maji kwa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, hivi sasa mji wa Karatu unapata huduma ya maji inayotolewa na kusimamiwa na taasisi mbili za KARUWASU na KAVIWASU. Hivyo, Serikali inao mpango wa kuanzisha taasisi moja na imara itakayotoa huduma ya maji kwa ufanisi kwa eneo lote la mji wa Karatu. Taasisi hiyo itapata ruzuku kwa kuzingatia miongozo iliyopo.