Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza: - Mheshimiwa Naibu Spika, je, Serikali ina mpango gani wa kuzijenga kwa kiwango cha lami barabara nyingi nchini zilizokwisha kufanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina?

Supplementary Question 1

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa majibu ya kuridhisha.

Kwa kuwa barabara nyingi hapa nchini zimeshafanyiwa upembuzi yakinifu kwa muda mrefu sasa na hizo barabara zimeshakuwa ni nyingi sana; na bado ukiuliza unaambiwa tunatafuta fedha kwa ajili ujenzi.

Je, Serikali haioni kwamba imefika wakati sasa tusitishe kwanza kuendelea kufanyia upembuzi yakinifu tumalize hizi barabara ambazo tayari zimeshajengwa ili resource tulizonazo tumalizie hizi zilizojengwa ndipo tuendee kufanya upembuzi yakinifu?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, iko barabara inayotoka Masasi kwenda Nachingwea mpaka Liwale zaidi ya kilometa 158, barabara hii imeshafanyiwa upembuzi yakinifu zaidi ya miaka minane sasa.

Je, ni lini Serikali wataijenga barabara hii kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Zuberi Kuchauka, Mbunge wa Liwale kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ni maelekezo ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi kuzifanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina barabara ambazo tunaendelea nazo. Lakini pia naomba nimwambie Mheshimiwa Mbunge kwamba moja ya mahitaji ili barabara ziweze kujengwa kwa kiwango cha lami ni kujua gharama zake ili hata wakati Serikali inatafuta fedha inakuwa inafahamu gharama ya zile barabara, inakuwa inafahamu ni wananchi gani ambao watapisha ujenzi, lakini pia inasadia kuzuia wananchi wasijenge maeneo ambako barabara itapita.

Kwa hiyo, tutaendelea kufanya usanifu ili kuwa tayari tunapopata fedha tuanze kujenga badala ya kusubiri kuanza usanifu pale tunapokuwa tumepata fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la pili, barabara aliyoitaja ya Masasi – Nachingwea hadi Liwale, katika bajeti hii tumetenga fedha kwa ajili ya kuanza kuijenga barabara kuanzia Masasi kwenda Nachingwea na Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili kipande cha Nachingwea kwenda Liwale, ahsante.

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza: - Mheshimiwa Naibu Spika, je, Serikali ina mpango gani wa kuzijenga kwa kiwango cha lami barabara nyingi nchini zilizokwisha kufanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina?

Supplementary Question 2

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi.

Kwa kuwa Rais wetu mpendwa Samia Suluhu Hassan ameshasaini mkopo wa trilioni 1.2 ambao unahusisha ujenzi wa barabara kadhaa, viwanja kadhaa pamoja na barabara ya kwenda Ruaha National Park inayopita Jimboni Kalenga.

Je, ni lini sasa Serikali tutegemee kuona kazi zinaanza kutekelezeka? Ahsante sana.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante; napenda kujibu swali la nyongeza la Kiswaga, Mbunge wa Kalenga kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, World Bank wameshakubali kuijenga barabara ya kutoka Iringa kwenye Ruaha National Park na ni kati ya hizo fedha ambazo ni 1.7 trillion. Kwa hiyo, nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba suala hilo sasa kinachosubiriwa tu nikuanza taratibu za manunuzi. Ahsante.

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza: - Mheshimiwa Naibu Spika, je, Serikali ina mpango gani wa kuzijenga kwa kiwango cha lami barabara nyingi nchini zilizokwisha kufanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina?

Supplementary Question 3

MHE. DANIEL B. SILLO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali moja la nyongeza.

Kwa kuwa barabara ya Dareda - Dongobesh usanifu wa kina umeshakamilika; je, ni lini zabuni zitatangazwa ili ujenzi huu uanze mara moja?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sillo, Mbunge wa Babati Vijijini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba barabara ya Dareda - Dongobesh imeshakamilika kwa kufanyiwa usanifu wa kina. Kwa hiyo, kwa sasa Serikali ipo kwenye hatua za kutafuta fedha ili barabara hiyo iweze kujengwa kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza: - Mheshimiwa Naibu Spika, je, Serikali ina mpango gani wa kuzijenga kwa kiwango cha lami barabara nyingi nchini zilizokwisha kufanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina?

Supplementary Question 4

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kunipa nafasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na juhudi kubwa za Serikali ya Chama cha Mapinduzi kutujengea barabara ya mwendokasi kutoka Bendera Tatu mpaka Mbagala Rangitatu, lakini bado kuna changamoto kubwa katika maeneo ya Rangitatu.

Je, Serikali lini itakamilisha kujenga tena upya na vizuri kwa kiwango cha lami barabara kutoka Mbagala Kokoto - Rangitatu kwenda Kongowe - Mwandege? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kisangi, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Dar es Salaam kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli barabara hii imekuwa na changamoto kubwa hasa ya foleni na Serikali sasa imeiweka kwenye mpango barabara hii ili iweze kujengwa upya na kupunguza foleni kubwa ambayo ni adha kubwa sana kwa wakazi wa Mbagala kwenda Kongowe, ahsante.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza: - Mheshimiwa Naibu Spika, je, Serikali ina mpango gani wa kuzijenga kwa kiwango cha lami barabara nyingi nchini zilizokwisha kufanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.

Kwa kuwa barabara inayopitiwa na Mlima Kitonga ni barabara ambayo imekuwa ikipata ajali nyingi na imekuwa ikipitisha mpaka wagonjwa wanaopelekwa hospitali ya Muhimbili.

Je, Serikali sasa iko tayari kujenga kwa kiwango cha lami barabara mbadala ili kama magari yakichelewa kupita pale kwa siku mbili au siku tatu; barabara ya Mahenge - Udekwa inayokwenda kutokezea Ilula ili wananchi waweze kupita kama magari yamekwamwa muda mrefu? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ritta Kabati, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Iringa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimjulishe Mheshimiwa Mbunge, kwanza kumpongeza kwa kutoa hilo wazo na sisi kama Serikali tumelichukua ili kweli kwamba kunapotokea changamoto basi tuwe na alternative ya kuweza kupitisha hasa kama kutatokea suala la wagonjwa kama alivyosema. Ahsante.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza: - Mheshimiwa Naibu Spika, je, Serikali ina mpango gani wa kuzijenga kwa kiwango cha lami barabara nyingi nchini zilizokwisha kufanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina?

Supplementary Question 6

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza katika Wizara hii ya Ujenzi na Uchukuzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya kutoka Kiranjeranje – Nanjilinji mpaka Ruangwa ni barabara ambayo imenadiwa katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya 2020 mpaka 2025, lakini pia imeshafanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina.

Je, lini Serikali itatenga fedha au kutenga bajeti kwa ajili ya kujenga barabara hii kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kassinge, Mbunge wa Kilwa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi kwamba, azma ya Serikali ni kuzijenga barabara zote kwa kiwango cha lami na ndio maana tumeshaanza kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwa kuwa tayari tumeshaanza hiyo ni hatua na Serikali inaendelea kutafuta fedha ili tuweze kuijenga hiyo barabara kwa kiwango cha lami, ahsante.