Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 37 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 331 2022-06-03

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza: -

Mheshimiwa Naibu Spika, je, Serikali ina mpango gani wa kuzijenga kwa kiwango cha lami barabara nyingi nchini zilizokwisha kufanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Zuberi Mohamed Kuchauka, Mbunge wa Liwale kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, mpango wa Serikali ni kuzijenga kwa kiwango cha lami barabara zote zilizokwishafanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina. Mpango huo unatekelezwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha, ahsante.