Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA K.n.y. MHE. KASALALI E. MAGENI aliuliza: - Je, ni kwa nini Serikali isiyaondoe mazao ya choroko na dengu kwenye utaratibu wa stakabadhi ghalani kwani utaratibu huo umekuwa kero kwa wakulima na wanunuzi?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, kwa kuwa kumekuwa na changamoto nyingi sana kwenye huu mfumo wa stakabadhi ghalani; je, nini mpango wa Serikali sasa kutoa elimu kwa wakulima wa choroko na dengu kabla ya mfumo haujaanza?

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini la pili, mfumo wa stakabadhi ghalani unahitaji uwepo wa warehouse (maghala); nini mpango wa Serikali kuhakikisha kwamba wanaanzisha maghala katika halmashauri zote ambazo huu mfumo unakwenda kufanyakazi? Ahsante.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Pius Chaya kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika eneo la kwanza la kuhusu elimu, Wizara tumejipanga kutoa mwongozo ambao ndani yake pia unajumuisha masuala ya elimu na masuala yote ya muhimu kabla ya kuingia katika Mfumo wa Stakabadhi za Ghala. Lengo letu ni kutatua changamoto ambazo zimekuwepo na hivyo kupitia mwongozo huu utakuwa umetibu tatizo hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili kuhusu maghala, tunafahamu kwamba moja kati ya requirement kubwa ya stakabadhi za ghala lazima kuwepo na maghala. Katika bajeti yetu ambayo tumeisoma kupitia Wizara ni kwamba katika mwaka wa fedha unaokuja tunakwenda kujenga maghala mengi katika maeneo ya uzailishaji, lengo letu ni kuhakikisha kwamba nchi yetu inakuwa na maghala kuanzia katika ngazi za vijiji ambapo wanazalisha kwenda juu. Kwa hiyo katika eneo hilo, Serikali imeona imeona umuhimu na tumetenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa maghala.

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA K.n.y. MHE. KASALALI E. MAGENI aliuliza: - Je, ni kwa nini Serikali isiyaondoe mazao ya choroko na dengu kwenye utaratibu wa stakabadhi ghalani kwani utaratibu huo umekuwa kero kwa wakulima na wanunuzi?

Supplementary Question 2

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana, msimu wa kilimo cha mazao ya choroko pamoja na dengu wa mwaka 2021/2022 katika Mkoa wa Shinyanga wakulima wa dengu walipata changamoto kubwa ya kupatiwa fedha kwa wakati; na hii ni kutokana na mfumo mzima kutokuwa na maandalizi mazuri ya ulipaji wa fedha katika Vyama vya Msingi ambavyo vilinunua mazao haya kupitia Vyama hivyo vya Msingi; je, Serikali imejipanga vipi kuhakikisha kwamba fedha ziwe zinafika kwa wakati kupitia Vyama vya Msingi vilivyopo katika ngazi hiyo ya ushirika ili mradi kuondoa hata na changamoto hii ya wakulima wa dengu na choroko katika maeneo hayo?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Butondo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema katika majibu yangu ya awali, kwa kutambua changamoto hizi tumeamua kuja na mwongozo maalum ambao utawajumuisha wadau wote. Lengo la mwisho ni kuhakikisha ya kwamba mkulima anafaidika na mazao yake na tunaondoa changamoto hasa za ucheleweshaji wa malipo. Nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba ndani mwongozo huu tutakwenda kutatua changamoto zote zilizopo katika mfumo wa stakabadhi za ghala.