Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 37 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 330 2022-06-03

Name

Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA K.n.y. MHE. KASALALI E. MAGENI aliuliza: -

Je, ni kwa nini Serikali isiyaondoe mazao ya choroko na dengu kwenye utaratibu wa stakabadhi ghalani kwani utaratibu huo umekuwa kero kwa wakulima na wanunuzi?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Emmanuel Mageni Kasalali, Mbunge wa Sumve, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mfumo wa Stakabadhi za Ghala unawezesha uuzaji wa mazao kwa ubora na bei ya ushindani, kupata takwimu sahihi za uzalishaji za mauzo na kuchochea uzalishaji. Mathalani, katika msimu wa mwaka 2020/2021 jumla ya kilo 14,394,077 za choroko zenye thamani ya shilingi bilioni 18.7 ziliuzwa kwa mfumo wa Stakabadhi za Ghala ikilinganishwa na kilo 1,130,453 zilizouzwa katika msimu wa mwaka 2019/2020 katika Mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Simiyu, Tabora na Singida.

Mheshimiwa Spika, zao la choroko, dengu na mazao mengine yataingizwa kwenye mfumo wa stakabadhi kwa kuzingatia vigezo muhimu vya uwepo wa ghala, waendesha ghala, elimu kwa wadau wa mfumo na mazingira ya soko kwa wakati husika.