Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI aliuliza: - Mheshimiwa Naibu Spika, je, ni lini Serikali itakamilisha majadiliano na Kampuni ya Tanzania Leaf Tobacco ili iweze kurudi nchini kuendelea kununua tumbaku?

Supplementary Question 1

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, niendelee kumshukuru sana Rais na nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, wakulima hawa wa tumbaku wamekuwa wakipangiwa uzalishaji na makampuni na mwisho wa siku wanachozalisha kinakuwa kidogo tofauti na matarajio yao na hasa wakulima hawa wadogo; na wanachozalisha cha ziada mwisho wa siku kinashindwa kununuliwa na mwisho wake kinaitwa jina la makinikia; nini kauli ya Serikali? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali langu la pili, kumekuwa na makato makubwa sana ya upandaji wa miti kwa wakulima hawa wa tumbaku. Fedha nyingi zinaishia kwa makampuni hayo na nyingine zinaishia benki na mkulima anaondoka bila fedha na mfano tu tosha mwaka jana wakulima hawa wa tumbaku wameweza kukatwa zaidi ya dola milioni tatu za miti ambapo ni zaidi ya bilioni sita. Nini kauli ya Serikali ili hao wakulima sasa tuwawekee mazingira mazuri waweze kuzalisha kwa wingi na weweze kupata faida kubwa na Serikali yetu iweze kupata fedha za kigeni? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Emmanuel Peter Cherehani, Mbunge wa Ushetu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye eneo la kwanza ni kweli imekuwepo hiyo changamoto na ndiyo maana Serikali tumeendelea kuhakikisha kwamba tunafungua milango kuwaleta nchini wawekezaji wengi zaidi ili kupata soko la uhakika la tumbaku yetu. Nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge ya kwamba Serikali itaendelea kuweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha kwamba zao hili la tumbaku linapata soko la uhakika na wakulima mwisho wa siku tumbaku yao inanunuliwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili la kuhusu makato, hii ni concern ambayo Mheshimiwa Mbunge amekuwa akiisema mara kwa mara na tumeshamuelekeza Mkurugenzi wa Bodi ya Tumbaku, kukaa na wadau wote kuona namna bora ya uendeshaji wa shughuli ya biashara ya tumbaku ili mkulima anufaike na kila ambacho anakilima shambani.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba jambo hili tunalichukua kwa umakini mkubwa na tunaendelea kulifanyia kazi ili mwisho wa siku mkulima aweze kunufaika na tumbaku yake.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI aliuliza: - Mheshimiwa Naibu Spika, je, ni lini Serikali itakamilisha majadiliano na Kampuni ya Tanzania Leaf Tobacco ili iweze kurudi nchini kuendelea kununua tumbaku?

Supplementary Question 2

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo.

Mheshimiwa Naibu Spika, wakulima wa Bulamata AMCOS wa eneo la Mishamo walilima tumbaku zao na kuwauzia Kampuni ya Naile Leaf Limited wanaidai kampuni hiyo dola za Kimarekani 600,000. Ni lini Serikali itawasaidia hawa wakulima wadogo ambao wamedhulumiwa haki zao za kimsingi na walipewa leseni na Serikali?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge Moshi Kakoso kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuna madai ya wakulima dhidi ya hii kampuni, Mheshimiwa Waziri aliwaita makampuni yote yanayodaiwa na akatoa mwongozo wa malipo; moja kati ya kazi ambayo Mkurugenzi wa Bodi anaendelea kuifuatilia ni kuhakikisha kwamba wakulima hao wanalipwa lakini pia tumewapa sharti kwamba hatuta-renew leseni yao mpaka pale watakapokamilisha malipo ya wakulima.

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi kama Wizara ya Kilimo tunahakikisha kwamba tunasimamia kwa dhati ili wakulima hawa waweze kulipwa na jambo hili lipo ndani ya meza ya Mheshimiwa Waziri, kazi inaendelea kuhakikisha kwamba malipo haya yanafanyika.