Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 37 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 329 2022-06-03

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI aliuliza: -

Mheshimiwa Naibu Spika, je, ni lini Serikali itakamilisha majadiliano na Kampuni ya Tanzania Leaf Tobacco ili iweze kurudi nchini kuendelea kununua tumbaku?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Emmanuel Peter Cherehani, Mbunge wa Ushetu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kulitaarifu Bunge lako tukufu na wakulima wa tumbaku nchini kuwa mwekezaji mpya ambaye ni mzawa Kampuni ya Amy Holdings Limited imekamilisha taratibu za kuchukua shughuli zilizokuwa zinafanywa na Kampuni ya TLTC na ameshapewa leseni. Aidha, Kampuni ya Amy Holdings Limited imeanza kununua tumbaku ambapo inatarajiwa kununua tani 10,000 za tumbaku katika msimu wa mwaka 2022/2023 ambazo itazichakata katika kiwanda kilichopo Morogoro ifikapo mwezi Julai, 2022.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya wakulima wote nchini, ninapenda kumshukuru Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kufungua milango ya wawekezaji ambayo matokeo yake ni pamoja na kupatikana kwa mwekezaji huyu.