Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA aliuliza: - Je, ni lini mradi wa barabara wa kilometa 96 unaofadhiliwa na Benki ya Dunia utafika Mbogwe?

Supplementary Question 1

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa majibu ya Serikali, lakini naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Mbogwe ina barabara nyingi, ukizijumlisha upana wake ni zaidi ya kilometa 3,000, hivyo basi barabara nyingi mpaka sasa hazipitiki Mheshimiwa Naibu Waziri na wewe ni shahidi, tulishawahi kwenda pamoja kwenye hilo jimbo.

Je, ni lini sasa hizi barabara nyingine ambazo haziko kwenye mpango utanipa bajeti ili TARURA ya Mbogwe iweze kuzitengeneza?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; Wilaya ya Mbogwe ina madaraja manne na mpaka sasa hivi madaraja hayo hayapitiki, likiwemo Daraja na mpaka wa Bukombe, Kata ya Masumbwe ambalo linaunganishwa na Kata ya Bugerenga.

Naomba kujua sasa Mheshimiwa Naibu Waziri umejipangaje ili kuweza kunisaidia wananchi wangu waendelee kufaidika na Serikali hii? Ahsante sana.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Nicodemas Henry Maganga, Mbunge wa Jimbo la Mbogwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inajenga barabara hatua kwa hatua na ndiyo maana hatua ya kwanza Mji wa Mbogwe umeingizwa katika Mpango wa RISE. Hatua nyingine Mheshimiwa Rais alifanikisha kuongeza bajeti ya TARURA ambapo tunafika maeneo mengi. Kwa hiyo, hata hizo barabara ambazo zimebakia tutaendelea kuzijenga kwa kutenga fedha za bajeti katika kila mwaka wa fedha unaokuja.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu madaraja ambayo Mheshimiwa Mbunge ameainisha hapa vilevile lengo la Serikali kupitia TARURA ni kufungua barabara hususani katika yale madaraja mabovu yakiwemo hayo aliyoyataja. Kwa hiyo, tutaendelea kufanya tathmini na tutatenga fedha ili kuhakikisha kwamba yanajengwa kwa wakati, ahsante sana.