Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 37 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 327 2022-06-03

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA aliuliza: -

Je, ni lini mradi wa barabara wa kilometa 96 unaofadhiliwa na Benki ya Dunia utafika Mbogwe?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Henry Nicodemas Maganga, Mbunge wa Jimbo la Mbogwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ya Tanzania, kupitia Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) na Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS), inatekeleza Mradi wa Maendeleo ya Barabara kwa Ushirikishaji Jamii na Ufunguaji Fursa za Kijamii na Kiuchumi Vijijini (Roads to Inclusion and Socioeconomic Opportunities - RISE). Mradi huu utagharimu kiasi cha dola za Marekani milioni 350, ambapo, kiasi cha milioni 300 ni mkopo wa masharti nafuu kutoka Benki ya Dunia na milioni 50 ni mchango wa Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe ni miongoni mwa Halmashauri zitakazonufaika na Mradi wa RISE ambapo jumla ya kilometa 96 zinaratajiwa kujengwa. Kwa sasa TARURA ipo kwenye hatua ya manunuzi ya Mtaalamu Mshauri wa kufanya usanifu wa kina (detailed engineering design) wa barabara zilizopendekezwa. Ujenzi unatarajiwa kuanza ndani ya mwaka wa fedha 2022/2023 baada ya usanifu kukamilika, ahsante.