Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kutenga fedha za dharura kwa ajili ya barabara?

Supplementary Question 1

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza, lakini pia napenda kuipongeza Serikali kwamba sasa imeanza kutenga fedha za dharura kwa ajili ya barabara zetu za TARURA, naipongeza sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la kwanza, barabara ya kutoka Changarawe kwenda Kisada ambayo inapita maeneo ya Matanana na Bumilayinga kutokana na miti ambayo wananchi walipanda kwa wingi na sasa imekomaa, inatumika sasa na malori makubwa.

Je, Serikali iko tayari kuitazama barabara hii kwa macho mawili kwa sababu inaharibika mara kwa mara?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; tunafahamu kwamba na wewe Naibu Spika ni mmoja wa wanufaika wa Mradi wa DMDP kama utakuja kukamilika, na sisi watu wa miji 45 tuna Mradi wa TACTIC. Mimi na wananchi wa Mafinga tunapenda kufahamu, je, katika huu Mradi wa TACTIC ambao utanufaisha kata nyingi za pale Mjini Mafinga, Upendo, Isalavanu, Kinyanambo na kadhalika, je, unaanza lini kwa sisi wa tu wa Mafinga? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Cosato David Chumi, Mbunge wa Jimbo la Mafinga Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali iko tayari kuiangalia kwa umakini barabara ya Changarawe – Kisada ambayo Mheshimiwa Mbunge ameiainisha hapa ili tuhakikishe kwamba inafanyiwa matengenezo.

Mheshimiwa Naibu Spika, lini Mradi wa TACTIC utaanza. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kuwa Halmashauri ya Mji wa Mafinga Mjini ipo katika awamu ya tatu ya utekelezaji wa mradi huo ambao utaanza katika mwaka wa fedha unaokuja wa 2022/2023. (Makofi)

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kutenga fedha za dharura kwa ajili ya barabara?

Supplementary Question 2

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kupata tatizo la mafuriko, madaraja mengi ndani ya Wilaya ya Hai yaliezuliwa yakiwemo Madaraja ya Marire na Kikafu. Daraja hili limekuwa kero kubwa kwa wananchi jambo linalomlazimu Mheshimiwa Diwani Martin Munisi kila siku asubuhi kuamka kwenda kuwavusha watoto wa shule kwenye daraja hili.

Je, Serikali ni lini itakarabati madaraja haya?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Saashisha Mafuwe, Mbunge wa Jimbo la Hai, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa daraja hili lina changamoto nyingi, niwaagize TARURA Mkoa wa Kilimanjaro wafike eneo la tukio wafanye tathmini na kuchukua hatua za haraka ikiwemo kujenga daraja dogo la dharura ili eneo hilo liweze kupitika, ahsante sana.

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kutenga fedha za dharura kwa ajili ya barabara?

Supplementary Question 3

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana, Manispaa ya Mpanda nayo ni kati ya Manispaa ambazo zipo kwenye Mradi wa TACTIC. Naomba Mheshimiwa Naibu Waziri aniambie na sisi Mpanda ni lini tutaanza Mradi huu wa TACTIC?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Sebastian Kapufi, Mbunge wa Mpanda Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Manispaa ya Mpanda ipo katika Awamu ya Tatu ya Utekelezaji wa Mradi wa TACTIC ambao utaanza mwaka wa fedha 2022/2023, ahsante sana.