Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 37 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 325 2022-06-03

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza kutenga fedha za dharura kwa ajili ya barabara?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana na kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cosato David Chumi, Mbunge wa Jimbo la Mafinga Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia TARURA imekuwa ikitenga fedha za dharura sawa na asilimia tano ya bajeti ya fedha za Mfuko wa Barabara. Katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali imetenga shilingi bilioni 11.45 kwa ajili ya fedha za dharura za matengenezo ya barabara nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kutenga fedha ya dharura kwa ajili ya kufanya matengenezo na ujenzi wa miundombinu ya barabara kulingana na upatikanaji wa fedha. Lengo ni kuboresha mtandao wa barabara unaohudumiwa na TARURA.