Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 28 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 246 2022-05-23

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga soko la kisasa la mazao yatokanayo na uvuvi Wilayani Nkasi?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI, alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aida Joseph Khenani, Mbunge wa Nkasi Kaskazini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mpango wa Serikali ni kujenga na kuboresha miundombinu ya uvuvi ikiwemo mialo na masoko katika maeneo mbalimbali nchini. Kwa upande wa mwambao wa Ziwa Tanganyika unaojumuisha Wilaya ya Nkasi shughuli za uvuvi zinafanyika katika mialo ipatayo 239. Kati ya mialo hiyo, Serikali iliboresha mialo minne ya Kibirizi, Ikola, Muyobozi na Kirando katika Wilaya ya Nkasi ambapo Mheshimiwa Mbunge anawakilisha. Aidha, Serikali imejenga na kuboresha masoko mawili ya samaki ya Kibirizi na Kasanga Wilayani Sumbawanga. Pia kwa sasa Serikali inaendelea na jitihada za kuupandisha hadhi mwalo wa Kirando uliopo Wilaya ya Nkasi ili uweze kufikia hadhi ya kuwa soko la kisasa la samaki na mazao ya uvuvi. Ahsante.