Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 9 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 139 2023-09-08

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itamaliza kazi ya kuwapatia wananchi Vitambulisho vya Taifa?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Joseph George Kakunda, Mbunge wa Jimbo la Sikonge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kazi ya kuwapatia wananchi Vitambulisho vya Taifa ni endelevu kwa kuwa kila mwaka kuna wananchi wanaotimiza umri wa miaka 18 ambao wanastahili kupewa Vitambulisho vya Taifa. Aidha, wapo wananchi wanaopoteza vitambulisho au wenye vitambulisho vinavyoharibika na hivyo kuhitajika vingine.

Mheshimiwa Spika, wananchi ambao walitambuliwa lakini hawajapata vitambulisho vyao, Serikali inatarajia kuwapatia vitambulisho vyao ifikapo mwezi Machi, 2024, nashukuru.