Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 6 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 82 2023-09-05

Name

Omar Issa Kombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza:-

Je, lini Serikali itaweka Mdaki katika Bandari ya Dar es Salaam kwa meli za abiria na mizigo za Azam Sea Link ili kuondoa usumbufu na kero kwa abiria?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Omar Issa Kombo, Mbunge wa Wingwi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia TPA imenunua midaki mitatu kwa ajili ya kuimarisha shughuli za ukaguzi katika eneo la Azam Link na eneo la kuhifadhi mizigo (Baggage room) ambapo midaki miwili imeshafungwa eneo la kuingia na kutoka katika eneo la kuhifadhi mizigo (Baggage room) na mdaki mmoja utafungwa katika eneo la Azam Link. Aidha, kwa mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali kupitIa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA), imetenga fedha kwa ajili ya kununua midaki mingine, kwa ajili ya eneo la Lighter Quay na yadi ya magari (RORO Yard), ahsante.